ASKOFU GWAJIMA ASIMULIA YALIYOMKUTA BAADA YA KUKAMATWA POLISI

Baada ya jana Februari 11,2017 Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima kuachiwa na Polisi baada ya mahojiano yaliyodumu toka Alhamisi kituo cha Polisi kati Dar es salaam kufuatia sakata la dawa za kulevya, leo February 12 2017 akiwa kwenye Ibada kanisani kwake amesimulia.

"Nilienda moja kwa moja kwa Kamanda Sirro, nikamkuta na Manji, wakasema wewe na Manji tunakwenda kuwapima kwa mkemia mkuu wa Serikali, wale watu waliokuwa wanapima walikuwa wanapima kwa uwazi kabisa, wakapima vitu vyote majibu hamna chochote.

“Waliposema twende tukapime nilikuwa tayari, na mimi nilisema ndani yangu hata ukiona Pombe andika umeona dawa za kulevya, nikasema mimi sina tatizo twendeni nyumbani kwangu na mkikuta hata sigara andikeni ni dawa za kulevya, wakasachi na hawakukuta kitu”

Tazama video hapa chini akizungumza

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post