TUNDU LISSU: TUMEJIPANGA VIZURI KUKABILIANA NA RAIS MAGUFULI

Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu amesema kuwa vyama vya upinzani vimejipanga vizuri kwaajili ya kukabiliana na Rais Dkt. John Magufuli .


Amesema hayo katika Semina iliyowashirikisha viongozi wa vyama vya upinzani kutoka Mataifa 16 iliyofanyika Makao Makuu ya Chama hicho Kinondoni Jijini Dar es salaam, amesema wanapambana kuhakikisha uwanja wa siasa unakuwa sawa lazima wabadili staili ya kumkabili Rais Magufuli.


Lissu amesema watafanya siasa ikiwa Magufuli anataka ama hataki, ama wanavunja Sheria ama hawavunji” Akipiga marufuku shughuli za kisiasa, hatuwezi kwenda kanisani kuomba, hapana lazima kazi ziendelee katika aina nyingine”amesema Lissu.


Aidha, Lissu ameongeza kuwa katika Uchaguzi uliopita haukuwa wa haki na huru ambapo mawakala waliokuwa wakihesabu kura walikamatwa na kupelekwa polisi.


Hata hivyo ameongeza kuwa hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa kiongozi yeyote atakayefanya siasa anaonekana kama mhalifu na hukamatwa na kupelekwa mahakamani, hivyo hakuna Demokrasia bali kuna udikteta mkubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post