SERIKALI YATANGAZA AJIRA ZA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI

SERIKALI imetangaza kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika shule za sekondari ambao wametakiwa kupeleka nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari, vya taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.


Tangazo kwa Umma lililotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish lilisema vyeti vya sekondari vinavyotakiwa kuhakikiwa ni vya kidato cha sita.


Alisema ajira hizo ni kwa walimu wa Stashahada na Shahada za Mafunzo ya Ualimu wa Masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu mwaka 2015.


Alisema nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara kuanzia jana hadi Ijumaa ya Desemba 16 mwaka huu na yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa hatafikiriwa katika uajiri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post