MPIGA PICHA MAARUFU TANZANIA MPOKI BUKUKU AFARIKI DUNIA

Mpiga picha maarufu Mpoki Bukuku amefariki dunia leo katika Taasisi ya Mifupa (MOI), alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.


Taarifa zinasema Mpoki amefariki dunia mchana huu na alipokelewa jana usiku baada ya kupata ajali ya gari maeneo la Mwenge ITV.


Mpoki Bukuku amewahi kufanya kazi kama Mpiga Picha Mkuu katika gazeti la Mwananchi pia amewahi kufanya kazi magazeti kadhaa likiwemo Majira na Nipashe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post