BODI YA MIKOPO YAONGEZA MUDA KWA WADAIWA SUGU KULIPA MADENI YAO HADI DESEMBA 30,2016


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imeongeza muda kwa wadaiwa sugu kulipa madeni yao hadi Desemba 30, 2016.



Hatua ya Bodi inafuatia mwitikio chanya kutoka kwa wadaiwa ndani ya siku 30 za awali ambazo zinakamilika leo Desemba 14, 2016.


Akitoa taarifa ya kuongezwa kwa muda; Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi, Abdul_Razaq Badru amesema kuwa wadau wameomba kuongezewa muda kutokana na baadhi yao kukabiliana na changamoto za majukumu ya kazi na hivyo kushindwa kujitokeza ndani ya siku 30 zilizokuwa zimetangazwa awali.


Katika hatua nyingine, Bw. Badru amesema kuwa ndani ya siku za nyongeza Ofisi za Bodi ya Mikopo zilizopo Mwenge, jijini Dar es Salaam zitaendelea kuwa wazi kwa siku za Jumamosi, Disemba 17, 2016 na Jumapili, Disemba 18, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri ili kutoa fursa muhimu kwa wadaiwa wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao hawajaanza kurejesha mikopo yao kupata taarifa kuhusu madeni yao na kulipa.


Ili kuharakisha utoaji wa muhtasari wa deni la mdaiwa; mhusika aje na Majina yake kamili, Chuo alichosoma, Mwaka wa kuanza na wa kuhitimu, anuani yake ya barua pepe (email), nambari ya simu ya kiganjani, mwajiri wake na Check Number yake iwapo ameajiriwa serikalini.
‘Kuwa Mzalendo, Rejesha Mkopo wa Elimu ya Juu’


Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459165 au 0767 513208


Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
14/12/2016

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post