MBUNGE WA CHADEMA GODBLESS LEMA AKOSA DHAMANA TENA

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amekwaa kisiki kwa mara nyingine katika harakati za kuomba dhamana baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kutupilia mbali ombi la marejeo ya kesi yake na kushauri kuwa Mawakili wake wakate rufaa ya kupinga zuio la dhamana


Mawakili wa Lema leo walikuwa wakirusha karata hiyo kwa mara ya tatu baada ya mara mbili za awali mteja wao kushindwa kupata dhamana.


Lema amesota rumande tangu alipokamatwa Novemba 3, 2016 akiwa mkoani Dodoma na kusafirishwa hadi Arusha ambapo anashtakiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya Rais Dkt Magufuli.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post