Mtandao wa habari wa Sahara ambao ulikuwa wa kwanza kuripoti kuhusu kuachiliwa kwa wasichana wa Chibok umechapisha ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kuhusu ubadilishanaji wa wafungwa uliosababisha kuachiliwa kwao.
Maelezo bado hayajathibitishwa ,lakini mtandao huo unasema kuwa wasichana 18 wana watoto na kwamba walibadilishwa na makamanda wanne wa Boko haram .
Pia mtandao huo umeripoti kwamba wasichana hao wanaelekea mji mkuu wa Abuja.
Via>>BBC
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com
Social Plugin