Wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu Wa Acacia Bulyanhulu Wasafisha Mazingira Kijiji cha Ilogi-Kahama


Wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu Wa Acacia Bulyanhulu wamesherehekea siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya kazi ya kusafisha mazingira katika Kijiji cha Ilogi kilichopo katika Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.


Leo Juni 5, ni Siku ya Mazingira Duniani.


Akizungumza wakati wa zoezi la usafi kijijini hapo Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ilogi Christopher Galila amesema hatua ya wafanyakazi kusafisha mazingira ya kijiji ni funzo muhimu kwa wananchi wengine na kusema kwamba uchafuzi wa mazingira hautavumiliwa katika maeneo yoyote kijijini humo.



“Pamoja na kutusaidia kusafisha hii leo meneo mbalimbali kwenye vizimba vya uchafu ambavyo baadhi vimekuwa na taka kwa muda mrefu pamoja na soko letu, Mgodi umetupatia mapipa kumi na tano ya kutupia taka ambayo yatatusaidia katika siku za usafi za kila juma, kwani kijiji chetu kina utaratibu wa kukusanya na kukagua usafi wa mazingira kila siku ya Jumamosi.”



Naye Kaimu Meneja wa Ufanisi wa Mgodi wa Bulyanhulu Bwana Onesmo Kabeho amesema timu ya wafanyakazi imefurahi mwitikio wa wananchi walioungana na wafanyakazi kusafisha mitaa, mitaro, vizimba vya taka na soko la kijiji.



“Sisi leo tumefurahi sana kung’arisha maeneo mbalimbali kijijini hapa kwa kuondoa kero ya uchafu ambao ni hatari kwa mazingira, tunatoa mwito kwa wanajamii wote kutunza mazingira kwa njia mbalimbali ikiwemo kudhibiti takataka hasa plastic ili watoto wetu na vizazi vijavyo visipate athari ya uchafuzi wa mazingira wa sasa”.
Wafanyakazi wa Bulyanhulu wakikusanya uchafu kwenye mitaro katika kijiji cha Ilogi.
Mfanyakazi wa Mgodi wa Bulyanhulu Dennis Cowan akiwa amebeba pipa la taka wakati wa zoezi la kusafisha mitaa.

Usafi ukiendelea katika Mazingira ya Soko la asili katika kijiji cha Ilogi.

Wauzaji wa mboga mboga wakifurahia zoezi la usafi sokoni

Kaimu Meneja wa Ufanisi wa Mgodi wa Bulyanhulu Bwana Onesmo Kabeho akikabidhi mapipa 15 ya kutupia takataka kwa uongozi wa kijiji cha Ilogi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post