Madereva Wakaidi Agizo la Serikali la Kutopitisha Magari Yenye Uzito Mkubwa Daraja Jipya La Kigamboni

 
Siku chache baada ya Serikali kuzindua daraja jipya la Kigamboni jiji Dar es Salaam na kukataza Magari yenye uzito zaidi ya tani kumi kutopita katika daraja hilo baadhi ya madereva wasiofuata sheria wamekuwa wakikiuka agizo hilo na kuonekana kupita katika daraja hilo.
 

Akitekeleza majukumu yake Inspekta Hassan Amadi ambaye ni mkuu wa usalama barabani wilaya kipolisi Kigamboni amesema kwamba ifike kipindi madereva waache kuvunja sheria na kufuata maelekezo nakuwataka madereva wengine wanaovunja sheria sehemu mbali mbali hususani wanao tumia daraja hilo kufuata sheria zilizowekwa na kuepuka makosa kama hayo.
 

Naye dereva aliyevunja sharia akijaribu kujitetea amesema kwamba hkufahamu utaratibu mzima wa upitaji katika barabara hiyo hivyo anakiri kosa alilofanya nakuwasihi madereva wenzake wafuate sheria Barabarani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post