ANGALIA PICHA 24 -MKUU MPYA WA MKOA WA SHINYANGA ANNE KILANGO MALECELA AKITAMBULISHWA KWENYE MKUTANO WA VIONGOZI WA MKOA WA SHINYANGA


Leo Jumatatu ya tarehe 21.03.2016 mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela amekabidhiwa ofisi ya mkoa wa Shinyanga na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga.Kilango amechukua nafasi ya Rufunga baada ya kuteuliwa na rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli hivi karibuni.


Baada ya kukabidhiwa ofisi hiyo,Malecela alitambulishwa kwa viongozi mbalimbali wa serikali ngazi ya wilaya na mkoa,taasisi za kidini,waandishi wa habari na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani humo.Pichani ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga wakati wa zoezi la utambulisho-Picha zote na Kadama Malunde na Magdalena Nkulu-Malunde1 blog


Aliyesimama ni katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi akiwatambulisha wageni waalikwa katika mkutano huo wa kumtambulisha mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela(kushoto),kulia ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Kanali mstaafu Tajiri Maulid




Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akiwaaga viongozi mbalimbali wa mkoa wa Shinyanga wakati akimtambulisha Anne Kilango Malecela kuwa ndiyo mkuu wa mkoa wa Shinyanga



Rufunga alitumia fursa hiyo kuwatahadharisha watumishi wa umma wazembe kuchapa kazi na kuacha majaribio katika kazi kwani serikali ya awamu ya tano ni ya aina yake ni imedhamiria kuleta mabadiliko ya kweli kwa wananchi.Pichani ni wenyeviti wa halmashauri za wilaya za Mkoa wa Shinyanga



 Rufunga aliwataka watendaji kushirikiana na mkuu wa mkoa wa Shinyanga kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.Kulia ni mkuu wa wilaya ya Kishapu Hawa Ng'humbi akifuatiwa na mkuu wa wilaya ya Kahama Vita Kawawa



Rufunga aliyeanza kutumikia mkoa wa Shinyanga tangu Oktoba 04,2011 mpaka mwezi Machi Mwaka huu aliwapongeza waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga kwa kazi nzuri wanayoendelea kufanya kuutangaza mkoa wa Shinyanga na kuihabarisha jamii kuhusu mambo mbali yanayoendelea mkoani humo-Kulia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifuatilia kwa umakini hotuba fupi ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akiwaaga viongozi na wananchi wa Shinyanga




Mkutano wa utambulisho unaendelea...pichani mstari wa mbele ni wenyeviti wa halmashauri za wilaya katika mkoa wa Shinyanga



Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akimkaribisha mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela wakati wa mkutano huo wa utambulisho



Viongozi wa halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini



Mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela akizungumza wakati wa mkutano wa kutambulishwa kwake kwa viongozi mbalimbali wa mkoa wa Shinyanga.Kilango aliyejinadi kuwa mzoefu katika kazi za serikali na kuwatumikia wananchi akitolea mfano wa miaka 15 ya ubunge,aliwataka watendaji katika serikali kujitahidi kufanya kazi usiku na mchana kwani wananchi walio wengi ni maskini na wanategemea viongozi wachapakazi ili kuwaondoa katika hali hiyo.



Kilango alisema wananchi wanataka viongozi wachapa kazi ili kutatua changamoto zinazowakabili ikiwemo upungufu wa madawati katika hivyo akawaomba ushirikiano ili kuwaletea maendeleo wananchi-Kulia ni askofu wa kanisa katoliki Jimbo la Shinyanga mhashamu Liberatus Sangu akiwa na Askofu mkuu wa kanisa la AICT dayosisi ya Shinyanga Dkt John Kanoni Nkola wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini



Kushoto ni Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt Ntuli Kapologwe akiwa na wajumbe wengine wa mkutano huo



Mstari wa kwanza mbele-Viongozi wa madhehebu ya dini mkoani Shinyanga wakiwa ukimbini



Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela alitumia fursa hiyo kuwaomba watendaji wa serikali wakiwemo wakuu wa wilaya na wakurugenzi kushirikiana naye katika kumaliza tatizo la upungufu wa madawati katika shule,kupiga vita mauaji ya vikongwe na albino na kuongeza kuwa mkoa huo hauna tatizo kubwa la wafanya kazi hewa



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na wakuu wa wilaya za mkoa wa Shinyanga ambazo ni Kishapu,Shinyanga na Kahama



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na viongozi wa vyama vya siasa



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na wenyeviti wa halmashauri 6 za wilaya mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na viongozi wa madhehebu ya dini



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na wakurugenzi wa halmashauri 6 za wilaya mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na makatibu tawala wa wilaya tatu za mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na sekretariati ya mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga



Picha ya pamoja,aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Ally Nassoro Rufunga(kushoto),mkuu wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela,katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi na baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga-Picha zote na Kadama Malunde na Magdalena Nkulu-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527