Picha 45!! TGNP MTANDAO YAENDESHA WARSHA YA SIKU MBILI SHINYANGA KUHUSU UCHAGUZI MKUU 2015 TANZANIA


Hpa ni katika ukumbi wa mikutano wa Katemi Hotel katika eneo la Ngokolo Mitumbani mjini Shinyanga ambako kumefanyika
warsha ya siku mbili ya kufanya tathmini ya mpango mkakati wa TGNP Mtandao wa kuwajengea uwezo wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu mwaka 2015 iliyofanyika mjini Shinyanga.Washiriki wa warsha hiyo wametoka katika mikoa ya Shinyanga,Mara na Simiyu.Washiriki wametumia fursa hiyo kujadili changamoto walizokabiliana nazo wanawake,vijana na watu wenye ulemavu katika uchaguzi uliopita na kujadili mikakati mbalimbali ya kufanikisha malengo yao katika chaguzi zijazo.


Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,ndugu Kadama Malunde amehudhuria warsha hiyo,ametuletea picha zifuatazo.....



Siku ya Kwanza-Februari 04,2016-Mwezeshaji wa warsha hiyo Dinah Nkya kutoka TGNP Mtandao akizngumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo ambapo alisema lengo kuu la warsha mrejesho hiyo ni kupima utekelezaji wa mpango kazi waliojiwekea washiriki baada ya mafunzo ya awali yaliyoanza mwaka 2014 kwa kuangalia namna walivyotumia nafasi zao,ushawishi wao katika kuelimisha jamii kuhusu ushiriki wa wanawake,vijana na walemavu katika mchakato wa uchaguzi na uongozi wa siasa.



Baadhi ya Washiriki kutoka mkoani Mara wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini



Baadhi ya washiriki kutoka wilaya ya Kahama wakiwa ukumbini



Baadhi ya washiriki kutoka manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini



Washiriki wakiwa ukumbini




Washiriki wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini





Mwezeshaji kutoka TGNP Mtandao Rebeca Mjema Kisena akizungumza katika warsha hiyo ambapo alisema katika uchaguzi mkuu 2015 wa madiwani,wabunge na rais kumekuwa na ongezeko la wanawake,vijana na watu wenye ulemavu katika nafasi za ubunge na udiwani kutokana na mradi wa uchaguzi wa TGNP mwaka 2014/2016 wa kuhamasisha makundi hayo kushiriki katika chaguzi mbalimbali





Washiriki katika warsha hiyo wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini



Mwandishi wa habari kutoka Radio Faraja Moshi Ndugulile akiwa ukumbini



Kushoto ni Mwezeshaji msaidizi kutoka TGNP Mtandao Ernest Mpalile akijaza dodoso wakati wa mahojiano na mmoja wa washiriki wa warsha hiyo ,Veronica Natalis kuhusu namna alivyoshiriki katika kutekeleza mradi wa uchaguzi



Kushoto ni Mwezeshaji wa warsha hiyo Dinah Nkya kutoka TGNP Mtandao akifanya mahojiano na mshiriki wa warsha hiyo Bonny Matto kutoka Tarime mkoani Mara




Siku ya Pili ya warsha Februari 05,2016-Wawezeshaji katika warsha hiyo kutoka TGNP wakiteta jambo ukumbini



Washiriki wa warsha hiyo wakifanya kazi za makundi



Mjadala unaendelea



Waandishi wa habari wakiwa ukumbini



Kushoto ni Mwezeshaji msaidizi kutoka TGNP Mtandao Ernest Mpalile



Washiriki wakiimba wimbo kuhusu usawa wa kijinsia



Tunaimba wimbo......




Washiriki wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini




Marco Mkanjiwa,ambaye ni mwenyekiti wa Shirikisho la watu wenye ulemavu wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga akizungumza ukumbini



Mraghabishi kutoka shirika la Sheria na Haki za Binadamu Tarime mkoani Mara ,Bonny Matto akiwa ukumbini





Mwezeshaji kutoka TGNP Mtandao Rebeca Mjema Kisena akizungumza ukumbini



Tunafuatilia kinachoendelea ......



Warsha inaendelea



Bwana Iddy Mpyalimi akichangia mada ukumbini





Mwandishi wa habari Moshi Ndugulile akieleza namna vyombo vya habari vilivyotumika kuhamasisha wanawake,vijana na walemavu kushiriki katika uchaguzi mkuu mwaka 2015





Mwandishi wa habari Masanja akizungumza ukumbini





Mkurugenzi wa Malunde1 blog,Fahari ya Shinyanga,bwana Kadama Malunde,akiwa ukumbini





Kulia ni bwana Marco Maduhu mwandishi wa habari gazeti la Nipashe akiwa na bwana Frank Mshana mwandishi wa habari ITV na Radio One





Washiriki wakiwa katika kazi ya kikundi





Washiriki wakiwa katika kazi ya kikundi




Kazi za makundi zinaendelea


Washiriki wakiwa katika kazi ya kikundi



Wawezeshaji wakiteta jambo ukumbini,kulia ni Dinah Nkya akiwa na Rebeca Mjema



Washiriki wakiimba ukumbini



Wawezeshaji na washiriki wa warsha hiyo wakiimba na kucheza ukumbini



Mshiriki wa warsha hiyo Marry kutoka manispaa ya Shinyanga akiwasilisha kazi ya kundi lake



Mratibu wa warsha hiyo bi Janeth Mawinza akizungumza ukumbini



Bwana Masanja kutoka mkoani Simiyu akiwasilisha kazi ya kundi lake


Bwana Bonny Matto kutoka mkoani Mara akiwasilisha kazi ya kundi lake



Kushoto ni mwezeshaji msaidizi kutoka TGNP Elieth Samwel Eliyuko,akifuatiwa na mwezeshaji msaidizi Ernest Mpalile na mratibu wa warsha hiyo Janeth Mawinza




Picha ya pamoja baada ya warsha kumalizika Februari 05,2016



Picha ya pamoja washiriki wote



Picha ya pamoja- Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527