Hatari!! MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AKUTANA NA AKINA MAMA ZAIDI YA 300 KUPAMBANA NA UGONJWA WA KIPINDU PINDU



Hapa ni katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambako wanawake/akina mama zaidi ya 300 wa manispaa ya Shinyanga wamekutana kujadili namna ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu ambao umeukumba mkoa wa Shinyanga.Mkutano huo umeitishwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Akina mama hao waliojitokeza kwa wingi leo jioni Oktoba 06,2015 wameweka mikakati mbalimbali ya kutokemeza ugonjwa kipindupindu ambapo Jana pekee wagonjwa 9 wamelazwa katika kambi maalum jirani na hospital ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ambapo kati ya hao 9 wawili wamefariki dunia.

Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog alikuwepo eneo la tukio ametusogezea picha 38..Angalia hapa chini




Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mkutano wake na wanawake zaidi ya 300 katika manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine alisema wanawake ni jeshi kubwa na ni walimu wakubwa katika familia hivyo wana nafasi kubwa ya kupambana na kipindu pindu kwa kuimarisha na kuhamasisha usafi kwa akina baba,watoto na hata wanawake wenzao.
"Kipindu pindu ni hatari sana...kinaua lazima tupambane nao kwa nguvu zote..nimewaita ili kila mmoja ajue Shinyanga tuna janga..sasa kila mtu achukue hatua,ugonjwa huu unatokana na uchafu..akina mama mna nafasi kubwa sana katika hili...."alisema Matiro.


Akina mama wakiwa wamenyoosha mikono...kwamba wako tayari kupambana na kipindupindu.....




Mkuu huyo wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliwaeleza akina mama hao kuwa chanzo cha ugonjwa huo ni uchafu yaani kula au kunywa kinyesi cha mtu mwingine hivyo ili kuhakikisha ugonjwa kipindu pindu ni vyema wananchi wakajenga vyoo,kuepuka kunywa maji yasiyochemshwa,kula vyakula vya moto,kuosha matunda kabla ya kula sambamba na kuepuka kunywa pombe za kienyeji.


Afisa afya mkuu wa manispaa ya Shinyanga Elly Nakuzelwa akizungumza wakati wa mkutano huo ambapo alisema ugonjwa huo unazidi kuenea kwa kasi katika manispaa ya Shinyanga ambapo jana pekee wagonjwa 9 walifikishwa katika kambi maalum ya wagonjwa wa kipindu pindu jirani na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga.


Afisa afya huyo alisema ili kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa katika manispaa ya Shinyanga tayari wamepiga marufuku tabia ya akina mama lishe na baba lishe kutembeza vyakula mtaani,unywaji pombe za kienyeji,kuzuia matanga kwenye familia yoyote iliyopatwa na kifo pamoja na kula vyakula kwenye sherehe yoyote.


Afisa afya mkuu wa manispaa ya Shinyanga Elly Nakuzelwa aliwataka wakazi wa Shinyanga kufika haraka hospitali pindi wanapoona dalili za ugonjwa wa kipindupindu ikiwemo kuharisha na kutapika mfululizo.


Mkutano unaendelea





Nakuzelwa aliwataka wananchi kujenga tabia ya kufunika vyoo vya shimo,kuepuka kula vyakula kwenye mikusanyiko ya watu wengi,kuacha kutembeza vyakula mtaani,kuuza vyakula shuleni,kununua mboga zinazouzwa chini badala ya kwenye meza.


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza juu ya matumizi ya vyoo majumbani kwani chanzo kikubwa cha ugonjwa wa kipindupindu ni kunywa au kula kinyesi cha mtu mwingine baada ya kuchanganyikana na vyakula ama maji anayokunywa binadamu.


Akina mama kutoka manispaa ya Shinyanga wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini ambapo walikubaliana kuimarisha usafi ili kutokomeza ugonjwa hatari wa kipindupindu



Miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kipindu pindu zilizotajwa ukumbini ni pamoja na kuharisha na kutapika mfululizo.


Meza kuu wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini



Akina mama wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini



Viongozi mbalimbali wa mitaa katika manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye mkutano wa akina mama katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga



Mmoja wa akina mama hao akichangia mawili matatu katika mkutano huo



Katika mkutano huo pia ilibainika kuwa wananchi wengi mjini Shinyanga hawana vyoo hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu



Wanawake hao pia walisisitizwa kujenga tabia ya kuwaelimisha wanaume juu ya umuhimu wa kujenga vyoo



Mkutano unaendelea



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumzia kuhusu amani ya nchi ambapo alisema serikali imejipanga vyema kukabiliana na watu waliojiandaa kufanya vurugu ikiwemo kuzuia wanawake na wazee wasipige kura siku ya uchaguzi mkuu nchini utakaofanyika Oktoba 25,2015.


Wanawake hao pia walihamasishana kushiriki uchaguzi mkuu ujao huku wakiiomba serikali kuimarisha ulinzi kwao na wazee kwani kumezuka uvumi kuwa kuna watu watawazuia kushiriki uchaguzi Oktoba 25 mwaka huu



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akawahamasisha wanawake kushiriki katika shughuli za maendeleo badala ya kutegemea wanaume...akasisitiza juu ya umuhimu wa kujiunga katika vikundi vya wajasiriamali ili serikali iweze kuwasaidia kwa urahisi zaidi badala ya kufuata mtu mmoja mmoja



Akina mama wakisikiliza kilichokuwa kinajiri ukumbini



Mkutano unaendelea



Mkutano unaendelea



Mkutano unaendelea



Maendeleo bila amani ni kazi bure...akina mama wakahamasishana kushiriki kulinda amani ya nchi....



Hakuna kutishana siku ya uchaguzi...mkuu wa wilaya ya Shinyanga akawahakikishia ulinzi siku ya uchaguzi huku akiwataka kulinda kadi zao za kupigia kura.




Wanawake na maendeleo ndiyo makubaliano waliyoafikiana.....



Mkutano unaendelea



Mkutano unaendelea



Mkutano unaendelea



Mkutano unaendelea


Afisa mtendaji kata ya Shinyanga Mjini Mathias Masalu akizungumza katika mkutano huo

Mwenyekiti wa mtaa wa Kaunda Joha Mussa akifunga mkutano huo


Akina mama wakitawanyika baada ya mkutano



Kila mmoja na njia yake...kushoto ni Mama Steve na Marietha William wakirudi kwao

Picha zote na Kadama Malunde- Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post