Tanzia!! MWENYEKITI WA DP MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI





Gari aliyopata nayo ajali Mch.Christopher Mtikila





Mchungaji Mtikila enzi za uhai wake


Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba mwenyekiti wa Chama cha DP nchini Tanzania mchungaji Christopher Mtikila amefariki dunia asubuhi hii Majira ya saa 12 kasorobo katika ajali katika Kijiji cha Msolwa karibu na mji wa Chalinze barabara ya Morogoro mkoani Pwani.


Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Jafari Ibrahim amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu wengine watatu waliokuwa katika gari hilo wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.


"Kwa maelezo ya dereva,gari ndogo ,waliyokuwa wanasafiria iliacha njia wakiwa wanaelekea jijini Dar es salaam,ikapinduka,ilikuwa na watu wanne akiwemo dereva na mchungaji Mtikila,hawa watatu ni majeruhi na mchungaji Mtikila inasemekana amefariki,mwili wa marehemu na majeruhi wako njia wakielekea hospitali ya Tumbi",amesema Kamanda Ibrahim.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post