Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Duh!! ANGALIA PICHA MKUTANO MKUBWA WA LOWASSA LEO MUSOMA MJINI...WANANCHI WENYE MAHABA NAYE WADEKI LAMI....


Mji wa Musoma na viunga vyake vyote umelazimika kusimama kwa muda kupisha mkutano mkubwa wa kampeni nuliokuwa ukiongozwa na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA Mh.Edwrad Lowassa
amevunja rekodi mjini Musoma.

Ilikuwa ni siku iliyoulazimu mji wa Musoma kusitisha shughuli zake huku barabara zikipigwa deki kwa ajili ya Edward Lowassa.

Katika siku yake ya pili ya kampeni akitumia chopa alimehutubia mikutano mikubwa sita tofauti iliyohudhuriwa na idadi kubwa zaidi wananchi huku akiahidi kuboresha miundombinu ya maji, afya, elimu, kuukarabati uwanja wa ndege wa mji huo, ikiwa ni pamoja na kufufua matumani ya ujenzi wa chuo kikuu ndani ya mji wa Musoma.

Fredrick Sumaye waziri mkuu mstaafu licha ya kutoa ya kutosha ya namna watanzania wanavyoweza kumpa ushindi Edward Lowassa, amesema siri kubwa ya maendeleo ya Tanzania ni kukinyofoa madarakani chama cha CCM.
Angalia picha nyingi hapa chini



Msafara wa Mhe. Edward Ngoyai Lowassa ukiwa umezingirwa na umati watu wa Musoma akielekea uwanja wa Mkendo Musoma,Jumapili 11/10/2015


Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (Kulia) na Mhe. Vicent Nyerere wakiwasili katika viwanja vya shule ya msingi Mkendo Musoma leo Jumapili 11/10/2015





Vicent Nyerere akiongea na wananchi wa Musoma katika viwanja vya shule ya msingi Mkendo Musoma mjini,Jumapili 11/10/2015




“Wingi wenu ni ishara kubwa kuwa mnataka mabadiliko ya kweli, natambua mnayo matatizo mengi hapa, ninaombeni mtumie wingi wenu huu kunipigia kura, mbunge na madiwani ili tuweze kuleta mabadiliko, nasisitiza nipeni mgombea ubunge ili tushirikiane kukamilisha matatizo hayo ikiwamo barabara,” amesema Lowassa











































“Wanasema wewe mwizi, sisi huku tumesema tutamchagua mwizi na kumfungia Ikulu miaka 10 atumikie wananchi.”-Vicent Nyerere(Mwenyekiti wa Chadema Musoma Mjini)




“Lowassa wamekutukana sana na wengine wanasema wewe mgonjwa, sasa sisi tumesema Mkoa wa Mara tunamchagua mgonjwa ili ashughulikie masuala ya hospitali zetu kwa kuwa hilo ndilo tatizo kubwa".-Vicent Nyerere





“Rais ambaye akiweka sahihi mtu ananyongwa, sahihi yake inaruhusu nchi kuingia vitani, anazungumza kuwa atajenga Mahakama za kufunga wezi na mafisadi, wakati ukienda magereza waliojaa ni walala hoi… sisi watu wa Mkoa wa Mara tunasema hatuhitaji mahakama za mafisadi, tunahitaji hospitali bora,” alisema Nyerere.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com