Makubwa Haya !! HII NDIO KAMPUNI INAYOWAZUIA WAFANYAKAZI WAKE KUSHIKA MIMBA

chiii
Ripoti iliyotoka mwaka 2014 inayohusu idadi ya watu duniani ilionyesha China ina watu bilioni 1.3..Katika vitu ambavyo walivifanya ili kupunguza watu walipitisha sheria ya kila wanandoa mwisho wa kuzaa ni mtoto mmoja.
Kuna hii nyingine imetokea nchini humo ambapo kampuni moja imepanga kutoa masharti kwa wafanyikazi wake watakiwa kupata ruhusa kabla ya kupata watoto.
watu
Moja ya fukwe China ikiwa na idadi kubwa ya watu
Wanawake wote walio kwenye ndoa wanaofikiria kupata watoto lazima wawe wamefanya kazi kwa mwaka mmoja kwenye kampuni hiyo kabla ya kutuma kibali cha kukubaliwa kushika mimba.
Kama ikitokea umekiuka sheria hiyo atakayeshika mimba atatozwa faini na pia kushushwa cheo kama alikuwa nacho.
Shirika la utangazaji la China limekosoa vikali kampuni hiyo na kusema haina ubinadamu kwa wafanyikazi wake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post