VIKONGWE WA MIAKA ZAIDI YA 100 WAFUNGA NDOA,WALIKUWA WACHUMBA MIAKA 27..


 

Nani amesema umechelewa kuoa au kuolewa? kuna watu huwa na wasiwasi kuwa wamechelewa kufunga ndoa kwa madai umri umekwenda lakini kwa George Kirby na Doreen Luckie imekua tofauti kabisa baada ya kuamua kufunga ndoa wakiwa na umri mkubwa.



George mwenye miaka 103 na Doreen mwenye miaka 91 waliamua kutimiza ndoto yao hiyo ya siku nyingi kwa kufunga ndoa.

Wawili hao wamefunga ndoa baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa miaka 27 huku kila mmoja akisema hajutii kuchelewa kufanya maamuzi hayo.



Sherehe hiyo ya aina yake ambayo ilifanyika katika hotel ya Eastbourne, Kusini mwa Uingereza ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo ndugu na marafiki wa karibu wa familia hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post