Taharuki !! NJIWA MWENYE HIRIZI NA BARUA AZUNGUKA KWENYE BAR 26


  
  Timbwili la aina yake lilizuka mwishoni mwa wiki iliyopita baada njiwa aliyekuwa amefungwa hirizi na barua iliyokuwa imeandikwa kwa Lugha ya Kiarabu kuzunguka katika baa zipatazo 26 zilizopo Banana, wilayani Ilala, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kutoka eneo hilo, njiwa huyo alizunguka katika kila baa iliyopo eneo hilo na mwisho alitua jirani ya baa moja.
 
Kabla ya kutua katika paa za baa hizo, baadhi ya watu waliokuwa wakipata kinywaji walisema njiwa huyo alionekana kwa muda mrefu akiwa  anaruka na vitu vyeupe kwenye mbawa zake.
 
Mmoja wa wateja katika baa hiyo alisema licha ya kumuona ndege huyo hawakujali  na  badala  yake  walimkamata  na kumwondolea hirizi na karatasi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post