OFISI MPYA YA CHADEMA YAVAMIWA NA KUBOMOLEWA NA WATU WASIOJULIKANA


Watu wasiofahamika wamevamia ofisi mpya ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Tawi la Mburahati kwa Madoto jijini Dar es salaam na kubomoa ofisi hiyo bila ya kutoa taarifa yoyote kwa uongozi wa ofisi hiyo.


Mwandishi wa habari hizi amefika eneo la Mburahati kwa Madoto zilipo ofisi hizo za Chadema na kukuta upande wa mbele wa ofisi hiyon ukiwa  umebomolewa na baadhi ya vitu kuvunjwa  huku uongozi wa ofisi hiyo ya Chadema ukielekezea lawama kwa serikali ya mtaa wa Mburahati kwa madoto kwa kuhusika na ubomoaji huo pasipo kufuata taratibu za ubomoaji.
Akijibu tuhuma hizo afisa mtendaji wa kata hiyo ya Mburahati hiyo Bi.Scholastica Matinde amesema sheria hairuhusu kwa chama chochote cha siasa kuweka ofisi kwenye maeneo ya masoko kama ambavyo chama hicho cha Chadema kilivyofanya.
Via>>ITV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post