MBUNGE SUGU ASHINDA KESI DHIDI YA MZAZI MWENZAKE MWENYE KUVAA MAVAZI YA AJABU AJABU


Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) ameshinda kesi aliyomfungulia aliyewahi kuwa mchumba wake Faiza Ally ambaye pia ni mama wa mtoto wake wa kike aitwaye Sasha.

Kwa mujibu wa maelezo ya Faiza kupitia akaunti yake ya Instagram, mahakama imetoa hukumu ambayo ni mtoto achukuliwe na kulelewa na baba yake mzazi.
 
Sugu alimshitaki Faiza kwa madai kuwa hana maadili na ana hofia kuwa atamharibu mtoto wao, hivyo alitaka kumchukua mtoto kutoka kwa mama yake aishi naye.

Hiki ndicho amekiandika Faiza baada ya hukumu kutolewa:
“Sielewi Joseph ameshindaje kesi- ushahidi wa picha peke yake sioni kama unatosha mimi kupokonywa mtoto wangu,mtoto wangu ni mdogo sana ananihitaji sana, na sita rudi hata ikibidi kuuza kila nilicho nacho kwa ajili ya kusimamia hili.

"Sijapewa nafasi nimepelekwa mahakamani ijumaa na leo jumanne nimepewa hukumu/ mwanangu achukuliwe….. hapana ! sitarudi nyuma na haitakua rahisi ninakata rufaa na kutafuta wakili wa kunisimamia hili.

"Mwanangu anasoma vizuri anaishi vizuri na naamini kwenye mikono yangu yuko salama zaidi ya kokote/ yaani kuhusu kukosa kukaa na mwanangu ni bora kufa kuliko kuishi nikimuona sasha ana lelewa na mama mwingine ikiwa mimi mama yake niko hai na makini katika malezi ya mtoto wangu.
  
"Nina ndoto na mwanangu nyingi sana , nahitaji kuishi nae yeye ndio kila kitu kwenye maisha yangu/ nampenda sana mwanangu na sijashindwa kumlea.

"Naona uchungu sana kupelekwa mahakamani na kupokonywa mtoto wangu bila sababu za msingi . 
  
"Sitaogopa cheo chake cha ubunge kamwe ntasimama kama mama mwenye haki kwa mtoto wake …mungu naomba nielekeze.nisimamie na unihukumie huu ukatili ninao fanyiwa na baba sasha …..”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post