AKINA MAMA 500 WA KABILA LA KITATURU WAANDAMANA KUOMBA MIILI YA MAREHEMU HUKO MEATU

Zaidi ya akina mama 500 wafugaji wa kabila la kitaturu toka katika kata ya bukundi wilayani Meatu mkoani Simiyu wameandamana hadi kwa mkuu wa wilaya hiyo wakishinikiza kupewa miili ya vijana wao wawili waliouawa kwa kupigwa risasi na askari wa kampuni ya Mwiba Holding iliyowekeza katika pori la makao wilayani humo.


Akina mama hao wamefika mjini Meatu majira ya saa mbili asubuhi wakiwa ndani ya maroli na walipofika eneo la mjini Mwanhuzi makao makuu ya mji wa Maeatu waliteremka  na baada ya muda mkuu wa wilaya hiyo Erasto Sima akiongozana na baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo  aliowaomba warudi katika kijiji cha Bukundi kwenye makao makuu ya kata hiyo ili aweze kuongea nao lakini waligoma kata kata kurudi huko.
 
 
 
Baada ya viongozi wa akina mama hao kuwasihi ndipo walipokubalina kwenda kwenye uwanja wa shule ya msingi,Mwanuhzi ambapo waliandamana chini ya ulinzi wa polisi na walipofika hapo walianza kutoa kilio chao cha kutaka wapewe miili ya watoto wao na kwamba iwapo mkuu wa wilaya hatawasikiliza basi wataenda kumuona rais kwani wamechoka na manyanyaso ya mwekezaji huyo.
 
 
 
Mwenyekiti wa chama cha wafugaji nchini,George Bajuta ambaye pia alikuwepo katika mkutano huo amesema wafugaji hao wamekuwa wakiishi kama wakimbizi katika nchi yao na kwamba sasa imetosha na hawataendelea kuvumilia kuona wafugaji wakiuwawa kwa kupigwa risasi na mwekezaji huyo.
 
 
 
Akijibu malalamiko ya wafugaji hao mkuu wa wilaya hiyo amesema serikali imelishughulikia kwa kina suala hilo ikiwa ni pamoja na kuwakamata wahusika waliofanya tukio hilo ambapo pia bado wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo kauli ambayo hata hivyo akina mama hao waliipinga na kudai kuwa wa serikali ya wilaya imekuwa haiwatendei haki bali imekuwa ikimtetea mwekezaji kampuni ya mwiba.
 
 
 
Mbunge wa jimbo hilo Meshaki Opurukwa ameitupia lawama serikali kwa madai kuwa suala hilo limekuwa la muda mrefu na mwekezaji huyo amekuwa akiuwawa wafugaji na kutochukuliwa hatua.
 
Aidha  alimtaka mkuu wa wilaya hiyo kutangaza kuanzia leo kusikitishwa kwa shughuli za kampuni ya Mwiba katika pori hilo hadi muafaka wa miili ya watu hao ipatikane na pia ofisi ya mkuu wa wilaya iwape chakula akina mama hao ambao wamegoma kurudi majumbani hadi wapate miili hiyo kauli ambayo ilipingwa na mkuu wa wilaya hiyo kwa madai kuwa suala hilo linashughulikiwa.
 
 Via>>ITV
 
Hata hivyo hadi itv inatoka eneo la tukio hilo akina mama hao walikuwa bado wamepiga kambi katika uwanja wa shule hiyo ambapo wamesema kamwe hawataondoka na sasa wanajipanga kwenda kumuona rais ili kumueleza kilio chao.
 
Via>>ITV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post