ILIKUWA KAMA UTANI HIVI,D'BANJ AKABURUZWA MAHAKAMANI

Dbanj60
Hii ishu ilikuwa kama utani hivi, zikaanza stori kwamba D’Banj anadaiwa na jamaa mmoja Nigeria.. baadae tukasikia kwamba jamaa anayemdai ametishia kumshtaki.. leo hii story ina mwendelezo wake.


Henry Ojogho ambaye ni makamu Mwenyekiti wa Broron Group and MindHub Technologies amesema anaidai Kampuni ya DKM Media ambayo inamilikiwa na D’Banj kiasi cha kama Naira Mil.60 ambazo ukiziweka kwenye hela yetu ni kama Tshs. Mil. 600 hivi.. kesi ilifika Mahakamani na kuanza kusikilizwa Lagos Nigeria, March 30 2015.

Siku hiyo ya kwanza kesi kusikilizwa Mahakamani wote wawili, yani D’Banj mwenyewe pamoja na Henry hawakuwepo Mahakamani.

Kesi ilisogezwa mbele na itasikilizwa tena Mahakamani siku mbili zijazo, yani May 7 2015.. D’Banj ni moja ya mastaa makubwa wenye mafanikio Africa ambaye anafanya kazi za kimuziki Marekani chini ya lebo ya G.O.O.D Music ambayo inamilikiwa na rapper Kanye West.

Kwenye list ya mastaa wa muziki wenye utajiri mkubwa zaidi Africa D’Banj yuko #3.. Hili deni ni kweli kashindwa kulipa au ni nini kinaendelea hapo??

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post