Mtu
mmoja amefariki dunia baada ya kugongwa vibaya na treni wakati
akivuka reli na kisha viungo vyake kusambaa katika mtaa wa ujenzi
Manispaa ya Morogoro .
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema marehemu
alijulikana kwa jina moja la Mangi ambapo wameeleza kusikitishwa na
ajali kwa kuwa hii ni mara ya tatu watu kugongwa na treni katika maeneo
hayo na kueleza kuwa amarehemu alikuwa anavuka reli.
Naye mwenyekiti wa mtaa wa ujenzi Christopher Charles ameelezea
tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha tabia ya kupita kwenye njia ya
Reli kwani wataendelea kusababisha ajali zisizo za lazima ambazo
zingeweza kuepukika.
Askari wa jeshi la polisi wamefika katika eneo la tukio na
kuchukua mwili wa marehemu ambapo umehifadhiwa katika chumba cha maiti
katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.
Via>>ITV
Via>>ITV