Angalia Picha!! WATU 19 WAFARIKI KWA AJALI YA HIACE KUTUMBUKIA MTONI HUKO MBEYA,WALIKUWA 21!!
Friday, April 17, 2015
Watu 19 wamekufa na wengine wanne wamejeruhiwa baada ya gari aina
ya Hiace kuanguka katik eneo linaloitwa Uwanja wa Ndege , Kiwira Mkoani
Mbeya.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Bwana Ahmed Msangi amesema watu
18 wamekufa papo hapo na mmoja amefariki dunia akiwa njiani wakati
akipelekwa Hospitali ya Misheni ya Igogwe kwa matibabu.
Kamanda MSANGI amesema kulikuwemo abiria 21 kwenye Hiace hiyo na
miongoni mwa waliokufa ni dereva wa gari hiyo na ameongeza majeruhi
aliozungumza nao wamemweleza walimtaka dereva apunguze mwendo,lakini
hakupunguza mwendo.
Amesema kutokana na mgomo wa mabasi makubwa Mkoani Mbeya dereva
huyo alitumia nafasi hiyo kubeba abiria hao ambao walikuwa wanakwenda
mnadani.
Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya amethibitisha kutokea kwa ajali
hiyo na kusema kuwa chanzo chake ni mwendo kasi, huku akiwata madereva
kuwa makini barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
Hiace ikiwa mtoni Hiace ikiwa mtoni
Wasamaria wema wakisaidiana na polisi kubeba miili ya majeruhi na waliopoteza maisha
Habari zaidi zitawajia punde tutakapozipata Copy and WIN : http://ow.ly/KNICZ
Habari zaidi zitawajia punde tutakapozipata Copy and WIN : http://ow.ly/KNICZ
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com
Social Plugin