WEKA PEMBENI YA MTOTO WA BONGO KUFUNDISHA SEKONDARI, LEO KUTANA NA MTOTO WA AJABU KUTOKA INDIA

 

Amini usiamini mtoto mwenye umri wa miaka miwili ameweka rekodi ya taifa ya ulengaji shabaha kwa mishale nchini India.
 
Kulingana na vitabu vya kumbukumbu ya rekodi za taifa, Dolly Shivani Cherukuri kutoka Vijaywada katika jimbo la Andhra Pradesh aliweka rekodi ya kuwa mshiriki mwenye umri mdogo zaidi kusajili alama 200 katika mashindano yaliyoandaliwa Jumanne iliyopita.

Kulingana na jarida la Press Trust la India ,mtoto huyo alifuma mishale 36 kutoka umbali wa mita 5 na kisha umbali wa mita 7 na kujizolea alama 388.

Tukio hilo lilishuhudiwa na wachezaji wakongwe na maafisa kutoka idara ya kumbukumbu za michezo.

''kwa hakika tunajivunia matokeo haya ''alisema afisa wa shirikisho la mishale la India bwana Gunjan Abrol.

Dolly ambaye alizaliwa baada ya kupandikizwa kwa mbegu ya babake kufuatia kifo cha kakake katika ajali ya barabarani.

Kakake alikuwa mrushaji mishale wa kimataifa Cherukuri Lenin.

Babake Cherukuri Satyanarayana ,anasema kuwa Dolly alifunzwa kufuma mishale, tangu alipozaliwa.

Babake ni mmiliki wa klabu kimoja kinachofunza kurusha mishale.

Aidha aliiambia shrika la habari la AFP kuwa kitambo alikuwa amemptengezea uta na mishale nyepesi ilikukuza talanta ya mtoto huyo.

Sasa babake anasema kuwa anapanga kumshirikisha mwanawe katika mashindano kwa nia ya kumsajili katika vitabu vya rekodi za dunia za Guinness.
Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527