Hujafa Hujaumbika- MZEE HUYU ANATESEKA SANA,ANAHITAJI MSAADA WAKO


Mzee Samwel Lupilya (62) mkazi wa kitongoji cha Madukani kijiji cha Sakwe wilaya ya Bariadi mkoa wa Simiyu anayesumbuliwa na kansa tangu mwaka jana.
Anasema alikwenda hospitali ya wilaya ya Bariadi ambayo sasa ni hospitali ya mkoa wa Simiyu ambapo aliambiwa na madaktari kuwa ugonjwa unaomsumbua unatibiwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza.
Kama anavyoonekana pichani upande wa kulia wa uso,shingoni na kuna kidonda kikubwa sasa kuonekana kusambaa sehemu za mwili wake na kumsababishia maumivu makali.


Anasema baada ya kufika Bugando aliambiwa na wahusika wa hospitali hiyo kutoa shilingi Milioni moja na laki 6 kwa ajili ya matibabu ,pesa ambazo alidai hana akalazimika kurudi nyumbani kusubiri msaada kutoka wasamaria wema huku akionekana kukata tamaa ya kuishi.

Kama umeguswa na ugonjwa wa mzee huyu piga simu namba 0768140069 kwa ajili ya mchango wako

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post