Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BIL 36 KWA MWAKA 2015/2016

Awali mwenyekiti wa kikao cha baraza la madiwani wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila,ambaye pia ni naibu meya wa manispaa hiyo na diwani wa kata ya Ndembezi akifungua kikao hicho leo katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga
Madiwani wakifuatilia kikao cha kupitisha bajeti ya mwaka 2015/2016

Kikao kinaendelea

Kikao kinaendelea

Madiwani wakifuatilia kinachoendelea ukumbini

Kikao kinaendelea

Kulia ni mwenyekiti wa kikao hicho David Nkulila akifunga kikao hicho,kushoto kwake ni mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Festo Kang'ombe,wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Annarose Nyamubi
Waandishi wa habari wakiwa ukumbini


Halmashauri ya manispaa ya shinyanga imepitisha mapendekezo ya mpango  wa bajeti  zaidi ya shilingi bilioni  36  kwa  kipindi cha mwaka 2015/2016  kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Mapendekezo hayo yamepitishwa leo na baraza la madiwani katika kikao maalum cha bajeti kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga.

Akiwasilisha mapendekezo  ya bajeti hiyo katika baraza la madiwani mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Festo Kang’ombe amesema  katika mwaka wa fedha 2015/2016 lengo la manispaa ni kukusanya Shilingi bilioni 36.

Amesema kati ya pesa hizo shilingi bilioni 2.5 zitakusanywa katika mapato yake ya ndani halmashauri,ruzuku kutoka serikalini bilioni 24 na ruzuku kutoka nje ya nchi shilingi zaidi ya shilingi bilioni tisa.

Kang’ombe amefafanua kuwa katika kipindi cha mwaka 2015/2016 Halmashauri hiyo inatarajia kukusanya  zaidi ya shilingi bilioni mbili kutoka katika vyanzo vyake vya ndani kiasi ambacho ni sawa na ongezeko la asilimia kumi na nne ikilinganishwa na makisio ya shilingi bilioni mbili na milioni mbili katika  mwaka wa fedha 2014/2015.

Aidha mkurugenzi huyo amesema sehemu kubwa ya ongezeko la mapato hayo ya ndani yanatarajiwa kukusanywa  kutokana na  kodi za ardhi,ada ya viwanja,ushuru wa mazao,ada ya minada, pamoja na leseni za biashara.

Na Kadama Malunde-Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com