BABU AMLAWITI MJUKUU WAKE WA MIAKA 13,AMHONGA SHILINGI ELFU 2 ASITOE SIRI!!



Polisi wilayani Masasi mkoani Mtwara inamshikilia mkazi wa kijiji cha Maili Sita kata ya Mtandi, Daudi Pilipili (44) kwa tuhuma za kumlawiti mjukuu wake wa kike mwenye umri wa 13.
Mkuu wa Polisi wilaya ya Masasi, Azaria Makubi alisema inadaiwa alitenda kosa hilo juzi saa 9:00 katika kijiji cha Maili Sita huku bibi wa mtoto akiwa amekwenda nyumbani kwa mwalimu wa shule anakosoma mjukuu wake (aliyelawitiwa) kwa mazungumzo.
Alisema siku ya tukio mzee huyo alimkamata mjukuu wake na kumwingiza chooni huku akimweka vitambaa mdomoni asitoe sauti na alipomaliza kitendo chake hicho cha kinyama alimpatia mtoto Sh 2,000 ili asitoe siri kwa wazazi wake.
Inadaiwa watoto wenzake ndio waliotoa taarifa hiyo baada ya kushuhudia kitendo hicho kikifanyika na polisi kutaarifiwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post