UKAWA WATANGAZA RASMI KUWA WATASUSIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA TANZANIA

UMOJA wa Kutetea katiba ya Wananchi UKAWA  umesema utasusia zoezi la upigaji wa kura  wa  Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la katiba inayotarajiwa kupigwa mwezi wa nne mwaka huu  kwa Madai Rais Jakaya Kikwete amekiuka makubaliano na Vyama vya siasa waliokubaliana mwaka jana mjini Dodoma.

         Azimio hilo limetangazwa leo Jijini Dar Es Salaam  na Mwenyekiti   mwenza wa Umoja wa vyama Vikuu vya Upinzani vinavyounda Umoja wa kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA Freeman Mbowe, wakati wa mkutano na Waandishi wa habari ambapo amesema Umoja huo hauwezi kuwepo katika mipango ya kuingamiza nchi wakati wa kupitisha katiba isiyokuwa na chembe yeyote ya kumsaidia mtanzania.
 
“Tunasema kwa pamoja hatutoshiriki katika katika kura za wa kupitisha katiba ya Chama Cha Mapinduzi,katiba iliyotengenezwa bila ya kuwa na maridhiano ya Kisiasa,maana Rais Kikwete ameamua kwa maksudi kabisa kutusaliti sisi viongozi wenzake wa kisiasa,tulikubaliana kwamba Bunge lile lisitishwe kutokana na kutoweza kupatikana kwa katiba mpya lakini alivyotoka pale akatusaliti na kuendelea na Bunge lile lilotafuna pesa za wananchi walalahoi”alisema mbowe.
 
     Mbowe aliongeza kuwa katika makubaliano hayo walifikia maazimio ya kufanyia mabadiliko katiba iliyopo ya mwaka 1977 katika vipengele mbalimbali ikiwemo kipengele cha kuwepo tume huru ya uchaguzi lakini Rais Kikwete akawageuka dakika za mwisho.
 
      Mbowe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Hai alizidi kusema kwa uchungu kwamba Umoja huo umebaini rafu mbalimbali wananazozifanya Chama cha mapinduzi ili katiba iliyopendekezwa iwe katiba harala kwa kuwasafirisha watu kutoka Mkoa wa dare s Salaam hadi Visiwani Unguja na pemba ili wakati wa kupiga kura ya kupitisha katika Iliopendekwa na bunge waipigie kura ya ndio ambapo Mbowe anasema wao hawatakubali.
 

    Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha NLD Dk. Emmanuel Makaidi amesema chama chake kitazunguka nchi nzima kuhamasisha wananchi kutopigia kura katiba pendekezwa kwa Madai Katiba hiyo ina mapungufu kibao na itazidi kuwaweka katika mazingira magumu yenye kujaa umasikini.
 
  Naye Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia alisema  anashangaa kitendo cha Rais Kikwete kuwageuka na kuyatupia mbali  makubaliano yao waliosema mchakato usitishwe mpaka baada ya uchaguzi mkuu na kufanyia marekebisho ya Katiba iliyopo na kusema kitendo hicho kinaonyesha kiongozi huyo alivyokuwa kigeugeu na umoja huo  hautokubali.
 
  Vilevile Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahimu Lipumba alisema Katiba wanayoitaka kuipitisha kinguvu haina mshiko kwa watanzania na imekaa kwa ajili ya kuwanafaisha watawala walioko madarakani,na akasema chama chake hakitokubali kuwepo katika dhambi ya kuwahujumu wa Tanzania  na wao watasusia mchakato huo.
 
 Vyama  Vinavyounda UKAWA  ni CUF,Chadema,NCCR mageuzi na NLD
 Na Karoli Vinsent-Dar es salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post