Mahakama moja nchini Ujerumani imempa idhini mwanamume mmoja kujisaidia haja ndogo akiwa amesimama baada ya mwenye nyumba kutaka alipwe akidai kuwa sakafu ya bafu lake iliharibiwa na mkojo wa mpangaji wake.
Mwenye nyumba ambaye
alitaka kulipwa dola 2,200 kwa uharibifu uliofanyika, alidai kwamba
sakafu yake iliyotengenezwa kwa mawe aina ya Marble iliharibiwa na mkojo.
Lakini
jaji aliamua kwamba njia aliyotumia mwanamume huyo kujisaidia
inaambatana na tamaduni nyingi ,akisema kuwa mtu anapojisaidia akiwa
amesimama ni jambo la kaiwada sana.
Kuna mjadala nchini Ujerumani
kuhusu ikiwa wanaume wanapaswa kujisaidia haja ndogo wakiwa wanasimama
au wakiwa wamekaa kwenye choo.
Baadhi ya vyoo nchini Ujerumani
haviwaruhusu watu kujisaidia wakiwa wamesimama, lakini wale wanaoamua
kuketi chini huitwa "Sitzpinkler", ikimaanisha kwamba wao sio kama
wanaume na sio jambo la kawaida kwa wanaume kukaa wakiwa wanajisaidia
haja ndogo.
Jaji Stefan Hank alikubaliana na ripoti ya wataalamu
kwamba tindikali inayotokana na mkojo au Euric Acid, huharibu sakafu
nyingi za vyoo.
Lakini kwa kukamilisha amri yake, jaji alisema
kwamba wanaume wanaosisitiza kusimama wanapojisaidia haja ndogo, mara
kwa mara huvurugana na wenye nyumba lakini hawawezi kuamrishwa kulipa
ikiwa sakafu itaharibika.
Via>>BBC
Via>>BBC