Msanii
mkongwe wa filamu nchini, Vicent Kigosi a.k.a Ray amejipanga kufanya
filamu nyingi za kimataifa mwaka huu, huku akiweka bayana ataanza na
Ghana pamoja na Nigeria.
Ray amesema ndani ya mwaka huu ataweka pembeni kazi za ndani na kujikita kimataifa zaidi.
“Nimepanga
kufanya mambo mengi mwaka huu, lakini mwaka huu movie zangu zote
nitafanya International sitafanya movie yoyote ya hapa hapa kwa sababu
kama hapa nishafanya sana, kwahiyo movie zangu zote nitakazocheza mwaka
huu 90% nitacheza nje, kwahiyo kama kuna lolote ambalo litabadilisha
nitawajulisha, ni mapema sana kusema lakini kitu ambacho ninaweza kuweka
wazi ni nitaanza kazi na Nigeria na Ghana, ndani ya mwezi wa nne
nadhani kazi zitakuwa zimeanza,” alisema Ray.
Mipango hii ya Ray inaonekana kja baada ya mwanadada Wema kwenda Ghana na kufanya filamu na Van Vicker.