MUME AUA MKE WAKE KWA KUMKATA SHOKA, KISHA KUMTUPA MTONI KISA WIVU WA MAPENZI

Mwanamke aitwaye Maria Haule  mkazi wa Kijiji cha Muhukuru Songea vijijini mkoani Ruvuma  ameuawa kwa kukatwa na shoka kichwani  na mume wake aitwaye  Salvatory Ndimbo  na kisha mwili wake  kuutupa mto Mkurumo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela anasema chanzo cha  mauaji hayo ni ugomvi  wa kimapenzi ambapo marehemu Maria Haule mwenye miaka arobaini  alikuwa na uhusiano wa kimapenzi  na mwanaume mwingine aitwaye  Anzekula na kutaka kuachana na  mumewe  Salvatory Ndimbo mwenye miaka sitini.
Jeshi la polisi linaendelea kumsaka mume wa  marehemu Maria Bw. Ndimbo mbaye ametoroka baada ya kufanya unyama huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post