Kikosi
cha Timu ya Mpira wa Miguu cha Radio Free Africa kutoka Sahara Media Group Ltd
leo Jumamosi ,saa kumi jioni kinatarajia kushuka katika uwanja wa CCM Katoro
katika mechi kabambe itakayowakutanisha na timu ya watuma salamu wa Katoro
mkoani Geita.
Nahodha
wa timu ya RFA Bernard James (Cheza Kidansi) amesema watangazaji wa
Radio Free Africa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo
katika mechi hiyo.
James
ameongeza kuwa malengo ya mchezo huu kwanza ni kukutana na wadau wa radio free
africa ikiwa ni pamoja kujenga urafiki na kufahamiana kati ya watangazaji na
wasikilizaji (wadau)
Amesema
baada ya mchezo huo kikosi cha timu ya Radio Free Africa kinajipanga
kuwavaa wadau wa igunga tabora na baadaye kufuatiwa na wadau wa babati
manyara.
Akitoa
majina ya kikosi kinachokwenda kufanya mauaji hayo leo mkoani geita james
amesema ni pamoja na:
1.William
Bundala (Kijukuu cha bibi k)
2.Renatus
Kiluvia (Bizzo)
3.Jackson
Nyamsuka
4.Bernard
James (Captain)
5.Dady
James
6.Yusuph
Magasha.
7.Godfrey
Kusolwa
8.David
Azaria.
9.Emmanuel
Mkuwi
10.Wambura
Mtani(Cotinho)
11.Juma
Baragaza.
James
ameongeza kuwa wachezaji wasaidizi ni pamoja na,
1.Dj John Lyatuu.
2.Dalton Mgala.
3.Salehe Masesa.
4.Elia Migongo.
5.Steve Moyo Mchongi.
Mchezo huo utakuwa na kiingilio cha
shilingi 2000/= tu getini.
Hii si ya kukosa mwanawane!!!!