Nini malengo ya kujenga msikiti mkubwa kama huu?
Nusu ya eneo katika ghuba ya Algiers, jengo kubwa taratibu limeanza kuibuka kutoka ardhini.
Katika
sehemu moja kitakuwa chumba cha kuabudia cha Msikiti Mkuu wa Algiers.
Katika sehemu nyingine kutakuwa na mnara mrefu kuliko yote duniani,
ukiwa na urefu wa mita 265 kwenda juu.
Kutakuwa na shule ya korani, maktaba na jumba la makumbusho, na maeneo na bustani zenye miti ya matunda mbalimbali.
Wageni
watawasili katika magari, treni na hata boti. Jengo hilo,
litakalokuwa na uwezo wa kuchukua watu 120,000, litaunganishwa na
bandari katika bahari ya Mediterani katika njia mbili za mandhari ya
kutembea.
Msikiti
huu utakuwa wa tatu kwa ukubwa wa eneo duniani, kwa mujibu wa wataalam
wa majengo na kuwa msikiti mkubwa kuliko yote barani Afrika.
"Ni
moja ya miradi ya karne," amesema Ouarda Youcef Khodja, afisa
mwandamizi katika wizara ya nyumba na mipango miji, wakati alipotembelea
eneo hilo la ujenzi.
Bi
Ouarda amesema Rais Abdelaziz Bouteflika alitaka msikiti huo kuwa"Mnara
wa Uislam na kwa mashujaa wa mapinduzi ya Algeria" - vita vya kupigania
uhuru kutoka Ufaransa.
Lakini
pia unaamanisha kuwa ishara kwa siku za baadaye. "Mnara huu utakuwa
kitu cha kurejelea katika mapinduzi ya sasa-mapinduzi ya maendeleo ya
Algeria."
Kama
ilivyo kwa miradi mingine mikubwa, inayofadhiliwa kutokana fedha
inayotokana na mafuta, ujenzi wa msikiti huu unategemea wataalam na
wafanyakazi kutoka nje. Umebuniwa michoro na wataalam wa majengo wa
Ujerumani na unajengwa na kampuni ya ujenzi ya China iitwayo China State
Construction Engineering Corporation, ambayo ina mamia ya wafanyakazi
wanaoishi katika eneo la ujenzi.
Na
kama ilivyo kwa miradi mingine, mradi huu umechelewa kutekelezwa.
Wizara ya nyumba na mipango miji hivi karibuni ilichukua jukumu la
kusimamia ujenzi wa msikiti huo kutoka wizara ya masuala ya dini. "Mungu
akipenda", anasema Bi Youcef Khodja, kwa sasa utakamilika mwishoni mwa
mwaka 2016, japo hata hiyo tarehe, ujenzi utakuwa umechelewa kwa zaidi
ya mwaka mmoja kutoka muda uliokuwa umepangwa.
Vipimo
vya msikiti huo, na eneo lake na gharama yake inakadiriwa kuwa dola za
Kimarekani bilioni 1-1.5, ikionyesha kuwa ni kipaumbele cha serikali.
Sababu
moja ya kutekelezwa kwa mradi huu ni uungwaji mkono na Bwana Bouteflika
ambao utakuwa ukumbusho wa urais wake nchini Algeria.
Sababu
nyingine inaweza kuonekana kwa ushindani wa mara kwa mara na majirani
zake, Morocco. Msikiti wa Algiers utaupita kidogo msikiti wa Hassan wa
Pili ulioko Casablanca kwa ukubwa wa eneo na kwa urefu wa mnara.
Lakini
msukumo mkubwa huenda ukawa jaribio la serikali kujenga utambulisho wa
taifa kidini na kutangaza Uislam kwa kuweka udhibiti juu ya misikiti na
maimam wanaosalisha humo.
Jitihada
hiyo iliyoanza pamoja na harakati za uhuru mwaka 1962 na kupata dharura
na mgogoro wa kiraia na wapinzani wa Kiislam katika miaka ya 1990,
wakati huo serikali ilipoteza udhibiti wa baadhi ya misikiti kwa
wahubiri waliochochea upinzani dhidi ya utawala wa serikali.
Ni
kwa mantiki hiyo Algeria inajenga msikiti mkubwa wa kisasa, kitu
ambacho kilikuwa kinakosekana mpaka sasa - anasema Kamel Chachoua,
mtaalam wa Algeria wa masuala ya dini katika Taasisi ya Utafiti na Elimu
katika Ulimwengu wa Kiarabu na Kiislam mjini Marseille.
Uamuzi
wa kujenga msikiti huu ulikuwa "ukimaanisha kuwadhibiti wapiganaji wa
Kiislam. Ni wazo la kuunda Uislam wa kitaifa baada ya kitisho cha miaka
ya 1990 na kuundolea Uislam taswira mbaya na kuufanya kuwa karibu zaidi
na serikali na kupambana na misimamo mikali ya kidini."
Msikiti
huu una maana ya kuwa ishara muhimu katika sehemu ya Algiers ambayo
imeshuhudia vitendo vingi vya misimamo mikali ya kidini katika miaka ya
1990, amesema.
"ni
njia ya kuficha misikiti midogo na kuidunisha. Ni namna ya kusema:
'Tunapenda Uislam, lakini Uislama wa kisasa'. "Unaweza kujenga miskiti
midogo 1,000 lakini haionekani - haionyeshi kuwa serikali iko katika
mchakato wa kuonyesha udhibiti wake juu ya Uislam na kwamba inajivunia
Uislam."
Wazo
la kuhamasisha utaifa wa dini ya Kiislam ambayo inaondokana na itikadi
zenye misimamo mikali kutoka nchi za Ghuba au kwingineko linaonekana
katika jitihada za serikali za kutangaza na kushirikisha Sufi zawaya, au
sheria za kidini. Pia inajidhihirisha katika utaalam wa ujenzi wa
msikiti mpya wa Afrika Kaskazini, wenye mnara mmoja wa muundo wa pembe
nne.
Mnara
utakwenda juu ya eneo la Mohammedia, na juu ya mabaki ya ukoloni
uliopita nchini Algeria. Moja kwa moja nyuma ya eneo la ujenzi ni jengo
kubwa lililotumika kukaliwa na wachungaji wa kimisionari kutoka Ufaransa
waliojulikana kama "peres blancs, au white fathers". Chini kidogo ya
barabara ni eneo la kiwanda cha zamani cha mvinyo.
Msikiti huo umebuniwa kuwa ishara ya utambulisho wa Algeria mpya, lakini utambulisho huo bado unapiganiwa.
Baadhi
ya wakosoaji wanauona msikiti huo kuwa zaidi kuwa ishara ya maelewano
baada ya mgogoro na wanasiasa waislam kuliko kuwa njia ya kupambana na
wasilam wenye misimamo mikali.
"Kipaumbele
ni kusema: 'Angalia tulivyo nchi ya Kiislam," anasema Amira Bouraoui,
mfuasi wa vuguvugu la upinzani la Barakat. "Ni njia nyingine ya
kuwanyamazisha wapinzani wa Kiislam na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa
chupa."
Bi
Bouraoui hivi karibuni alitishiwa katika mtadao wa kijamii wa Facebook
baada ya kuuliza kama sauti ya vipaza sauti ingeweza kupunguzwa. Wananch
iwa Algeria wasiofungamana na dini wanaona hili kama mfululizo wa
mifano ya kufuatilia uislam na kukosekana kwa uvumilivu wa kidini.
Hata
hivyo kwa kawaida, iwapo Wa-Algeria wanaonekana kuwa watazamaji zaidi,
hiyo ni hali ya juu juu, anasema Nacer Djabi, mwana sociolojia katika
chuo kikuu cha Algiers. "katika kiwango cha kijamii si fikirii kama
wanadini hasa, anasema Djabi.
"Ni
watu wasiotaka mabadiliko sana, mabadiliko wanayoonyesha ni ya juu juu.
Unaweza kuona hilo katika mitaa ya Algiers - kuna wasichana wengi wenye
hijab, lakini hizo haziwazuii kuwa na wapenzi wa kiume, kunywa bia.
"Wa-
Algeria wengi, wafanyabiashara, wanakwenda Mecca, wanaswali mara tano
kwa siku", anasema."Lakini hali halibadili tabia yao kama wananachi kama
Waislam."
Kwa
upande wao wakazi wa Mohammedia wanaonekana kutofurahishwa na ujenzi wa
msikiti mkubwa katika maeneo yao, wakisema fedha hiyo ingetumika katika
mambo mengine.
"Unatakiwa
kuanza na elimu na afya, na baadaye unaweza kufikiria kuenzi dini,"
anasema Racim, mwanafunzi mwenye umri wa miaka 22.
"Katika mtazamo wa Kiislam, mahali pa kuswalia si muhimu sana - ni kile kilichoko moyoni."