Fumbo la siku zote kwamba wanawake
ni wanene kuliko wanaume limepata ufumbuzi...ni wanene kwani wanahitaji
mwili wenye umbo zuri na makalio makubwa ili kupata watoto waliojaaliwa
werevu.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa wanaakademia ambao wanasema
kuwa wanawake wenye makalio na mapaja makubwa na umbo zuri kutokana na
mafuta mfano kama
Kim Kardashian hupata watoto werevu.
Nini hasa kinawafanya
watoto wao kuwa werevu basi? Mafuta yanayopatikana katika sehemu za
mwili wa mwanamke huwa na manufaa makubwa sana kwa watoto hasa
wanapokuwa wananyonya, mafuta haya hupitia kwenye maziwa ya mama hadi
kwa mwili wa mtoto.
Profesa Will Lassek wa chuo kikuu cha
Pittsburgh University, Pennsylvania, aliyeongoza utafiti huo, anasema
mafuta yanayopatikana katika sehemu hizo za mwili, husaidia sana katika
kukuza ubongo wa mtoto mchanga.
'Unahitaji mafuta mengi ya
mwilini ili kuwa na mfumo mzuri wa neva na mafuta katika sehemu hizi za
mwili yaani mapaja na makalio, huwa yana madini yajulikanayo kama DHA
(docosahexaenoic acid), ambayo ni muhimu sana katika kutengeza ubongo wa
binadamu.
Inaonekana kama wanawake wameweza kujua mbinu za kuhifadhi mafuta katika sehemu hizo za mwili hadi wanapopata mtoto.
Kwa
mda mrefu haijajulikana kwa nini wanawake wanakuwa wanene
sana.......mafuta ya mwili wao yakiwa ni asilimia 30 ya uzani wa mwili.
Professa
Lassek anasema kwamba mafuta hayo ni kiwango sawa na yale
yanayopatikana katika wanyama kama Dubu au Nyangumi wanapojiandaa kuzaa.
Wanasayansi
wanasema mafuta yanayopatikana katika mapaja na makalio ya wanawake
ndio yanayotumika kutengeza ubongo wa watoto wachanga.
Mafuta
mengi katika mwili wa mwanamke huisha mwilini pindi mama anapomnyonyesha
mtoto wake, kulingana na Profesa Lassek, aliyechapisha utafiti wake
katika kitabu chake kipya chenye kichwa ''Kwa nini wanawake wanahitaji
mafuta mwilini. ''
Wanawake wanaonyonyesha hupoteza kilo nusu ya mafuta mwilini kila mwezi.
CHANZO-BBC SWAHILI