Loredana Chivu ni mwanamitindo nchini Romania
Baba mmoja amejiua baada ya kuona picha za uchi
zamwanawe wa kike katika jarida la Playboy nchini Romania.
Loredana Chivu alirarua ukurasa uliokuwa na picha yake
akiwa 'amepoz' katika jarida hilo la Playboy na punde babake alipogundua kuhusu
picha hizo, alizongwa na mawazo na hata kumkana mwanawe.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mirror, msichana huyo mwenye
umbo la kuvutia alisema, '' babangu aliacha kuongea na mimi na kuonekana mwenye
hasira sana''.
"alipogundua kuwa picha hizo zilikua zangu,
alijitenga sana na kujaribu kunitenga na mimi''.
Nilidhani labda angesahau na sikudhani hata siku moja
angejitoa uhai.
Loredana
Chivu anasema anajuta sana kwani babake hakuwahi kuongea naye baada ya kupata
picha zake
Mwanamitindo huyo Loredana
Chivu mwenye mamia ya picha akiwa nusu uchi kwenye akaunti yake ya Instagram,
alikuwa na uhusiano wa karibu sana na babake lakini alisema yote hayo
yalibadilika baada ya babake kuona picha zake akiwa nusu uchi.
Alipokwenda kumtembelea
babake miezi michache baadaye, baada ya kuamua kwamba kimya kilikuwa
kimeendelea kwa muda mrefu sana, alishtuka sana kumpata babake akiwa amejitoa
uhai
"nilipata akiwa na
kamba shingoni akiwa ananing'inia chumbani''.
Loredana,anayeishi nchini
Romania, anasema kuwa tangu kifo cha babake, amekuwa akiwaza na kuwazua kwamba
aliamua kujiua kwa sababu ya mgogoro kati yetu na hasa kuhusu picha zangu
zilizoziona kwenye jarida la Playboy.
''Najuta sana kwamba
hakuwahi kupata muda wa kuzungumza na babangu kuhusu yaliyotokea''.
''Hakuacha ujumbe wowote
kabla ya kujitoa uhai, siku zote tulikuwa na uhusiano mzuri lakini yote
yalibadilika baada ya baba kuona picha zangu nikiwa uchi. Bado inaniuma sana na
singemtakia mtu yeyote kupatwa na kama yaliyonikuta''.