Hii inatoka Nigeria, Sunday Osemwekhe alifikishwa
Mahakamani kwa kosa la mauaji na amekubali kwamba alifanya kosa hilo,
lakini chanzo cha ugomvi wao ilikuwa shutuma alizompa kaka yake kwamba
alimuibia supu.
Ugomvi ukaenda mbali zaidi, Osemwekhe
aliamua kuchukua panga na kumjeruhi kaka yake huyo sehemu mbalimbali za
mwili, ambapo baada ya kufikishwa Hospitali alifariki kutokana na
majeraha makubwa.
Uchunguzi wa Polisi Nigeria umeonyesha
kuwa mtuhumiwa alishikwa na hasira baada ya kuangalia supu yake aliyoiacha kwenye sufuria ya supu na kugundua haikuwa kama alivyoiacha,
mzozo ukaanza kati yake na kaka yake, hasira zilipozidi Osemwekhe alichukua panga na kumpiga kaka yake na kumsababishia majeraha makubwa.
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba +255 688 405 951