Mwanamme mmoja aliyefahamika kwa jina la Simeo Isaka (42),mkazi wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela tarafa ya Mweli wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, ameuawa kwa kukatwa na jembe kichwani wakati akishangilia matokeo ya ushindi wa mgombea wake kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha, alisema tukio hilo limetokea Desemba 15 majira ya saa saba usiku wakati mwanamme akishangilia matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa.
Kamanda Kamugisha alisema, marehemu huyo alikuwa akishangilia ushindi wa mgombea wa Chama Cha Demokrsia na Maendeleo (Chadema), ngazi ya mwenyekiti wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela wilayani Kahama.
Kamanda Kamugisha alisema wakati Simeo Isaka akishangilia ushindi huo ghafla alivamiwa na watu watatu wasiojulikana kisha kumkata jembe kichwani, na kisha kukimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama ambako alipoteza maisha.
Kamanda Kamugisha alisema jeshi la polisi linafanya uchunguzi kuhusu tukio hilo na juhudi za kuwasaka na kuwakamata watuhumiwa wa tukio hilo zinaendelea ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>MAGAZETI
Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>MAGAZETI