Breaking News!! APASULIWA KICHWA BAADA YA KUPAMIA FUNGU LA VITUNGUU KATIKA MNADA WA TINDE-SHINYANGA

Habari tulizozipata hivi punde kutoka mnada wa Tinde ulioko katika kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga, ambao hufanyika kila siku ya Jumanne ni kwamba mwanamme mmoja ambaye jina lake halijafahamika mara moja anadaiwa kupasuliwa kichwa na wananchi waliokuwa eneo la mnada.


Mdau wa Malunde1 blog  Paul De Nyoso Seseja aliyepo eneo la tukio anasema tukio hilo limetokea jioni hii na limetokana na mwanamme huyo kupamia/kuparamia fungu la vitunguu vilivyokuwa vinauzwa katika soko hilo kitendo ambacho kiliamsha hasira kwa watu waliokuwa eneo hilo baada ya mtuhumiwa aliyeonekana kulewa pombe kuonesha ubabe baada ya kuulizwa kwanini kapamia vitunguu hivyo


Mwanamme huyo akiwa ameanguka chini baada ya kupigwa kwa fimbo na wananchi katika mnada wa Tinde ambapo inadaiwa kuwa amepasuka kichwa
Wasamaria wema wakitoa msaada kwa mwanamme huyo kabla ya kumkimbiza katika zahanati ya Tinde kwa ajili ya matibabu



Safari kuelekea zahanati ya Tinde

Picha zote na  Paul De Nyoso Seseja-Mdau wa Malunde1 blog Tinde

Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>MAGAZETI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527