MTOTO WA MIAKA MIWILI AUA MAMA YAKE DUKANI

 
Maafisa nchini Marekani wanasema kuwa mtoto mmoja mdogo mvulana wa miaka miwili amempiga risasi kimakosa mama yake mzazi na kumuua ndani ya duka moja kubwa la uuzaji bidhaa la Wal-Mart.


Maafisa wa usalama wanasema bunduki iliyotumika iliyokuwa imefichwa ilichomoka wakati mvulana huyo alipokaribia na kuligusa begi la mkononi la mama yake mwenye umri wa miaka 29.

Tukio hilo limetokea katika mji wa Hayden, katika jimbo la Idaho.

Msemaji wa Kaunti hiyo anasema mwanamke huyo alikuwa na kibali cha kumiliki silaha.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527