KUMBE AISHA MADINDA AMEFARIKI KWA KUDUNGWA SINDANO YENYE MADAWA YA KULEVYA

Marehemu Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’enzi za uhai wake.

MENGINE yameibuka! Kifo cha aliyekuwa mnenguaji wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’ kimeibua mengine ambapo baadhi ya watu wa karibu wanaamini kimetokana na kudungwa sindano tano za majimaji yenye madawa ya kulevya, ‘unga’ na rafiki yake.

Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Aisha alidungwa kwa makusudi sindano hizo na rafiki yake mmoja ambaye polisi bado wanamtafuta, ikidaiwa lengo lilikuwa kummaliza.

YALIYOSEMWA

Akizungumza kwenye msiba wa mnenguaji huyo nyota nyumbani kulikokuwa na kilio, Kigamboni jijini Dar, mwombolezaji mmoja ambaye ni mtu wa karibu na marehemu alisema:


“Unajua siku za karibuni, Aisha alirudia kubwia unga kama zamani, sasa majuzi mimi nilikutana naye akasema yuko kwa rafiki yake, Mwananyamala (Dar), lakini huyo rafiki aliyenitajia ni mmbwia unga mkubwa na amekuwa akiwadunga sindano wenzake.

Marehemu Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’enzi za uhai wake.

Stori:waandishi wetu MENGINE yameibuka! Kifo cha aliyekuwa mnenguaji wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’ kimeibua mengine ambapo baadhi ya watu wa karibu wanaamini kimetokana na kudungwa sindano tano za majimaji yenye madawa ya kulevya, ‘unga’ na rafiki yake, Ijumaa ‘Kubwa’ linakupa zaidi.


Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Aisha alidungwa kwa makusudi sindano hizo na rafiki yake mmoja ambaye polisi bado wanamtafuta, ikidaiwa lengo lilikuwa kummaliza.


YALIYOSEMWA

Akizungumza kwenye msiba wa mnenguaji huyo nyota nyumbani kulikokuwa na kilio, Kigamboni jijini Dar, mwombolezaji mmoja ambaye ni mtu wa karibu na marehemu alisema:


“Unajua siku za karibuni, Aisha alirudia kubwia unga kama zamani, sasa majuzi mimi nilikutana naye akasema yuko kwa rafiki yake, Mwananyamala (Dar), lakini huyo rafiki aliyenitajia ni mmbwia unga mkubwa na amekuwa akiwadunga sindano wenzake.


“Sasa si unajua kwamba, sindano zile ukidungwa bila kipimo ni sumu mwilini. Uwezekano ni mkubwa kwamba, sindano alizodungwa na mwenzake ndizo zimechukua uhai wake,” kilidai chanzo hicho.


CHANZO KINGINE

Kwa mujibu wa chanzo kingine msibani hapo, upo wasiwasi kwamba tangu Aisha arejee Bongo akitokea Dubai kuna mtu amekuwa akimtishia maisha kwamba atamtoa roho.


Chanzo hicho kilidai kwamba, staa huyo ambaye alirudi akiwa vizuri amekuwa akipewa vitisho na mtu huyo bila kutaja sababu.


SIKU YA KIFO

Siku ya tukio, juzi Jumatano, habari zinadai kwamba, Mkurugenzi wa Vipindi wa Radio Clouds FM, Ruge Mutahaba alipigiwa simu na daktari mmoja wa Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kinondoni, Mwananyamala na kuambiwa kuwa, kuna mwili wa mtu anayefanana na Aisha Madinda umetelekezwa hospitalini hapo na watu wasiojulikana na wameondoka.


Baada ya taarifa hizo, Ruge alimwendea hewani Bosi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka na kumjulisha madai ya daktari.

“Asha Baraka alikuwa Kigoma. Kwa hiyo alipopewa taarifa hizo alimpigia simu kiongozi wa wanamuziki wa Twanga Pepeta, Luiza Nyoni Mbutu na kumpa maelekezo kwamba afuatilie habari alizoambiwa na Ruge kama ni kweli.”



AISHA MADINDA NDANI YA MOCHWARI

Ikazidi kudaiwa kuwa, Luiza na wanamuziki wenzake, Lilian Tungaraza ‘Lilian Intaneti’ na Maria Soloma walifunga safari hadi Mwananyamala na kuukuta mwili wa Aisha ukiwa tayari mochwari, wakamjulisha Asha ambaye  alifunga safari na machozi juu kurejea Dar.



MTOTO WA MAREHEMU, ANAITWA NAOMI


Akizungumza na gazeti hili ndani ya Hospitali ya Mwananyamala muda mfupi baada ya mwili wa mama yake kuingizwa mochwari, binti wa Aisha, Naomi  huku akimwaga machozi, alisema:


“Mama alikuwa akiishi Kigamboni siku za karibuni. Mimi pia nikaamua kwenda kuishi naye.”


Akaendelea: “Kuna kama siku tatu nyuma mama hakuwa akilala nyumbani, jana (Jumanne sasa), asubuhi mama alinitumia meseji akisema anaomba nimtumie pesa, nikamtumia.


“Lakini juzi, Jumatano mchanamchana nilisema nimpigie simu mama nimuulize huko aliko anaendeleaje? Kabla sijafanya hivyo, mama mkubwa alinitumia meseji na kuniambia mama amefariki dunia, ndiyo nikaja huku.”



KIKAO CHA FAMILIA AELEZEA KIFO CHAKE!

Binti huyo aliendelea kusema kuwa, siku za karibu, marehemu aliwahi kuwaita ndugu zake na kuwapa ujumbe wa ajabu.


“Kuna siku aliwaita ndugu zake nyumbani akasema katika familia yetu wote, mimi ndiyo nitakayeanza kufa. Sijui mama alijua atakufa ndiyo maana akasema vile,” alisema binti huyo.


MASWALI YA MSINGI

Mpaka sasa maswali ambayo yalitawala msibani ni haya! Je, ni nani aliyeufikisha mwili wa marehemu Hospitali ya Mwananyamala na kuutelekeza? Je, dokta alijuaje kuwa alikuwa Aisha Madinda?


Je, mwili wake ulipelekwa hospitalini hapo na mtu mmoja au wengi? Walitumia usafiri gani? Bajaj au teksi? Ni vyema pia polisi wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar wakafuatilia kifo hiki kwa undani.


VIA GPL

Mpenzi Msomaji,Tunapenda kukutumia Habari zetu zote mara tu Tunapoziweka Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post