Vurugu ya aina yake imetokea kwenye ofisi
za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Shinyanga Mjini baada ya Chama Cha Demokrasia
na Maendeleo Chadema kushinda kwa kishindo katika kata ya Ngokolo hali
iliyosababisha viongozi wa ngazi za juu wa CCM kuanza kushikana uchawi kwamba
nani kasababisha anguko hilo.
Malunde1 blog inaambiwa kuwa jana majira ya saa tano asubuhi katibu
wa siasa na uenezi wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Charles Shigino almanusura atwangane makonde na kuishia kutukanana matusi ya nguoni na katibu wa umoja wa
Vijana wilaya ya Shinyanga Mjini (UVCCM), Zawadi Hussein.
Varangati hilo lilitokea wakati Shigino
akiingia katika ofisi za chama hicho ambapo ghafla alitokea katibu wa umoja wa
vijana (UVCCM Hussein na kumzuia kuingia katika ofisi hizo na kuanza kumrushia
maneno machafu akimtuhumu kuchangia kufanya vibaya katika kata ya Ngokolo ambapo Chadema
wamepata ushindi katika mitaa 6 na CCM wakiambulia mtaa mmoja pekee.
“Wakati naendelea kujitetea, aliendelea kuniporomoshea matusi mfululizo ,ndipo uzalendo ukanishinda na mimi nikaanza kujihami na kusababisha
ugomvi mkubwa nje ya ofisi ya chama, na kujaza umati wa watu waliofika kushuhudia
ugomvi huu, ambao hauna maana zaidi ya kukiaibisha chama”,Shigino aliiambia
Malunde1 blog.
Katibu wa umoja wa Vijana wilaya ya
Shinyanga Mjini Zawadi Hussein amesema alimzuia Shigino kuingia katika ofisi za
chama hicho kwa madai kuwa yeye ni msaliti wa chama na amekuwa akitoa siri za CCM na
kuzipeleka kwa wapinzani.
Katika uchaguzi huo wilaya ya Shinyanga
Mjini kati ya mitaa 55 CCM, wamepata mitaa 26, CHADEMA mitaa 29.
Kata iliyoleta kizaa zaa ni ile iliyokuwa inaongozwa na diwani Sebastian Peter Mzuka maarufu OBAMA ambaye alirubunika kisha kuhamia CCM ambako pia alivurugwa na kurudi Chadema akidai kuwa ndiyo chama chenye uleta ukombozi japokuwa mpaka sasa haajajibiwa na mamlaka zinazohusika juu ya hatma ya udiwani wao baada ya kuandika barua kuomba kurudishiwa udiwani wake na mwenzake Zacharia Mfuko kutoka kata ya Masekelo ambako pia mitaa yote imezolewa na CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika juzi.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>MAGAZETI
Kata iliyoleta kizaa zaa ni ile iliyokuwa inaongozwa na diwani Sebastian Peter Mzuka maarufu OBAMA ambaye alirubunika kisha kuhamia CCM ambako pia alivurugwa na kurudi Chadema akidai kuwa ndiyo chama chenye uleta ukombozi japokuwa mpaka sasa haajajibiwa na mamlaka zinazohusika juu ya hatma ya udiwani wao baada ya kuandika barua kuomba kurudishiwa udiwani wake na mwenzake Zacharia Mfuko kutoka kata ya Masekelo ambako pia mitaa yote imezolewa na CHADEMA katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika juzi.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>MAGAZETI