Inatisha!! POLISI WATUMIA MABOMU VURUGU ZA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO MOROGORO

Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>
polisi wakiwa kazini
Jeshi la Polisi limelazimika kutumia mabomu ya machozi  kuwatawanya  wananchi wa Dumila na  Mbigiri wilayani Kilosa mkoani Morogoro  baada ya kufunga barabara ya Morogoro Dodoma kwa kutumia mawe na kuchoma matairi barabarani katika eneo la dumila na  kusababisha abiria wanaotumia barabara ya Morogoro -Dodoma kukosa mawasiliano kwa zaidi ya masaa sita.




Waandishi wa Malunde1 blog wameshuhudia wananchi hao wakifunga barabara kwa mawe na matairi huku wengine wakionekana na mapanga ambapo wamesema wanalalamikia viongozi wa serikali ya kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya kufumbia macho mgogoro wa ardhi na kushindwa kuwachukulia hatua wafugaji wanaowazuia wakulima wasilime katika eneo la Mbigiri.



Vurugu hizo zilidumu kwa muda mrefu na juhudi za kudhibiti wakulima hao zimechukua muda baada ya askari wachache wa kituo cha Dumila kuonekana kuzidiwa nguvu ambapo baadhi ya wakulima wengine  wameonekana wakivamia wakuvunja nyumba za wageni zinazomilikiwa na wafugaji na kupora magodoro na vitu mbalimbali ambapo baadae  vikosi vya jeshi la polisi viliongezwa na kufanikiwa kudhibiti  baadhi ya watuhumiwa na kufungua barabara.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paul amesema chanzo cha vurugu hizo ni wazee zaidi ya kumi walizuiwa kulima katika mashamba yao mbigiri ambapo walipelekeka malalamiko yao kwa afisa tarafa ambapo wakiwa ofisini kundi la vijana walifika na kufunga ofisi wazee hao pamoja na afisa tarafa hadi walipofika na koOkolewa na jeshi la polisi na katika tukio hilo watu 20 wanashikiliwa  na jeshi la polisi.

Afisa tarafa na wazee walifungiwa ndani wakizungumzia tukio hilo wamesema kuna mgogoro wa siku nyingi kati ya wakulima na wafugaji na upo katika ngazi za juu huku wakieleza kusikitishwa na hatua za kufunga barabara na kuomba serikali kuingilia kati kutatua mgogoro wa ardhi uliopo.





Hata hivyo katika hatua nyingine Tunaambiwa Chanzo cha vurugu hizo kinadaiwa kuwa ni kukatwa mkono kwa mkulima mmoja aishie Kijiji cha Mketeni wilayani Kilosa wakati akibishana na mfugaji ambaye ni kabila la Kimasai kuhusu eneo la kulishia mifugo.

Kufuatia kitendo hicho cha kukatwa mkono, mkulima huyo aliwafuata wenzake na kuwapa taarifa ambapo walikusanyika na kuanzisha vurugu dhidi ya wafugaji wa eneo hilo.

Baada ya kuona kuwa bado haitoshi na baadhi ya wafugaji kukimbia, wakulima walimalizia hasira zao katika Barabara ya Morogoro - Dodoma ambapo waliamua kuifunga kwa takribani masaa mawili huku wakichoma matairi.

Kufuatia hali hiyo polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliingilia kati na kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wakulima ambao pia walikuwa tayari wamevamia baadhi ya nyumba za kulala wageni zinazomilikiwa na wafugaji eneo hilo na kufanya uharibifu.

Majeruhi katika vurugu hizo wamepelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.


Na waandishi maalum wa Malunde1 blog Morogoro

Mtandao Huu Unakujali,Ni Wako!! Tunataka Tukutumie Habari zetu Zote Mara Tu Tunapozipandisha Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa Sasa Hivi ><<VITUKO>>,"MAPENZI",<<HABARI MSETO>>

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post