WANANCHI WAHAMASISHWA KUWA NA DESTURI YA KUPIMA AFYA ZAO MARA KWA MARA



Wananchi wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kujenga desturi ya kupima afya zao mara kwa mara ili kusaidia kutambua afya zao  ikiwa ni pamoja na kupata  huduma na ushauri  juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Kauli hiyo imetolewa leo katika kijiji cha Mwime Kata ya Mwendakulima na mratibu wa Ukimwi wa halmashauri ya Mji wa Kahama Elibariki Minja wakati akizungumza kwenye mashindano ya kutafuta kikundi bora cha utunzi wa nyimbo zenye maudhui ya Ukimwi kuelekea siku ya Ukimwi Dunia Disemba mosi.

Amesema  kama wananchi watakuwa na mwamko wa kupima afya zao, itasaidia   jamii kutambua  madhara ya VVU, pamoja na kujua mbinu za kujilinda na kujikinga na maambvukizi mapya ya Ukimwi na kwamba  njia pekee ya kufikisaha elimu kwa wananchi ni pamoja na viongozi na mashirika kuendelea kutoa elimu.

Minja amewataka wananchi kutambua kwamba  wilaya ya Kahama  ndio inayoongoza kwa kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya Ukimwi katika mkoa wa Shinyanga,hivyo jamii haina budi kutambua madhara pamoja na mbinu ya kujilinda.

Kwa upande wake Afisa mahusiano wa Mgodi huo Davidi Kilala amesema lengo la kufanya mashindano hayo  ni kupata kikundi kitakachoelimisha  jamii juu ya ukimwi, jinsi ya kujikinga na maambukizi mapya ya ukimwi kwa pamoja na  unyanyapaa njia ya Sanaa.

Amesema tayari wamekwisha kupata kikundi cha Tuaminiane  ambacho kitaungana na vikundi vingine kutoka Mwendakulima na Chapulwa  kupata  mwakilishi wa kata hiyo atakayekwenda kuhamasisha kwenye maadhimisho ya  siku ya Ukimwi Duniani ambapo wilaya ya Kahama itafanyika katika kata ya  Lunguya katika halmashauri ya Msalala.

Kwa upande wake Kaimu Afisa mtendaji wa Kata hiyo  Marry Bukwimba  amewataka wananchi wa kata hivyo  kuzingatia ushauri unaotolewa na viongozi wa serikali na Mgodi wa Buzwagi  ili kupata jamii yenye ulelewa wa  kutambua mabaya na mazuri.

Nao baadhi ya  wananchi wametoa pongezi kwa Mgodi wa Buzwagi, kwa  kubuni hamasa ya vikundi katika vijiji ambapo wameomba serikali na wadau wengine  kujitokeza kuhamasisha ili jamii itambue   jinsi ya kujikinga na Maambukizi ya VVU.


Na Ndalike Sonda-Kahama

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527