Laana!! JAMAA APEWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KISA KUTAKA KULAWITI MTOTO WA MIAKA 8

ANGALIA PICHA KIJANA ALIYEPIGWA KWA TUHUMA ZA KUBAKA

Huyu ndiyo mtuhumiwa.


Alifika Nyumbani na kumlaghai mtoto(jina tunalo)kwa pipi na kumuita uncle, uncle Akamvuta mpaka vichakani na kutaka kuanza kumlawiti. Mtoto alipoona hivyo akaanza kupiga kelele na kupambana na mtuhumiwa.


Muasi alikuwa tayari ameshavua nguo, alipoona mtoto anapiga kelele akaanza kumng'ata na meno mashavuni na kumpiga na jiwe kwenye paji la uso.


Bahati nzuri, MUNGU saidia, kuna mama alikuwa anashusha matofali akaskia kelele hizo kabla ya tendo baya kufanyika.

 Akaita watu wakamkuta mtuhumiwa akiwa anaendelea kujaribu kumlawiti mtoto huyo wa kiume. Alifanikiwa kumwaga haja zake tu, ila hakufanikiwa kumuingia kimwili.

Watu wenye hasira walimpa adhabu yake na yeye, kabla Police hawajafika na kumtia mbaroni..

Inasemekana kuwa mtuhumiwa huyu ndio tabia yake, ila hii ndio ilikuwa arobaini yake. Mitaa ya Mbezi ya Kimara, amezunguka sana kuharibu watoto wa watu.

Kila Nyumba akifika anauliza baba na mama wapo?? akiambiwa tu hawapo anaanza shughuli zake.Hivi sasa yuko Hospitali ya TUMBI mahututi, akingojea kusomewa mashtaka.

Kama kuna lolote la ziada tutaendelea kufahamishana. 



Sura ya mtoto imefichwa kutokana na maadili


Huyu ni mtoto mwenye umri wa miaka 8, alikuwa nyumbani wakati wazazi wake wote wakiwa hawapo, Alikuwa yeye na kaka yake mwenye umri wa miaka 12.Ndipo swahibu lilipomkuta mpaka kufanya aumizwe kiasi hiki .






Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527