TAZAMA PICHA ZA YULE MCHAWI ANAYEMEZA MAPANGA, ALIYEKATAZWA KUINGIA DUBAI

Picha: Mwenye vipuli usoni na tattoo nyingi zaidi duniani azuiwa kuingia Dubai
Rolf Buchholz, Mjerumani anaetajwa kuwa mtu mwenye vipuli vingi zaidi usoni akiwa amejitoboa zaidi ya mara 100 usoni amekataliwa kuingia Dubai kutokana na sababu za kiusalama.
Rolf alikuwa amejipanga kufanya onesho la sarakasi na kikundi chake nchini humo ambapo huonesha michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ‘kumeza mapanga’.
Ameieleza Association Press kuwa maafisa wa uhamiaji walikuwa tayari wameshaweka stamp kwenye Passport yake na kumruhusu kuingia lakini alizuiwa baadae kabla hajavuka eneo hilo.
Club aliyokuwa amepanga kufanyia onesho hilo imeeleza kuwa, ilitumiwa barua pepe inayoeleza kuwa uongozi wa Uwanja wa ndege ulitaja ‘sababu za usalama’ kuwa chanzo cha katazo hilo.
Rolf Buchholz anatajwa kuwa mtu mwenye tattoo nyingi zaidi duniani.
Rolf Bushholz

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post