KUTANA NA GARI LISILOTUMIA MAFUTA KWA ZAIDI YA MIAKA 100,LINADUMU ZAIDI YA MAISHA YA MTUMIAJI WAKE


Moja kati ya mambo ambayo mtu wa anayafikiria kabla hajanunua gari ni kiasi cha mafuta kinachotumiwa na gari hilo. Lakini ukiwa na gari hili… unaweza usifikirie kabisa kuhusu mafuta huku ukilitumia kama kawaida kwa zaidi ya miaka 100.

Wataalam wa masuala ya magari wameeleza kuwa endapo gari linalotumia ‘Thorium’ litaanza kufanya kazi litakuwa gari ambalo linaweza kutumika kwa zaidi ya miaka 100 bila kuongezwa mafuta.

Kwa maana hiyo Thorium itakuwa na uwezo wa kudumu hata zaidi ya maisha ya mtumiaji wa gari hilo.

Kampuni ya Laser Power tayari imeshatengeneza idea ya kutumia Thorium katika engine za magari  ambapo wataitumia kitaalam kuchemsha maji na kuwa chanzo cha nguvu ya kuendesha gari.

Hata hivyo, CEO wa Laser Power System, Dr. Charles Sevens aliiambia Mashable kuwa engine za Thorium hazitaweza kuwa kwenye magari hivi karibu kwa kuwa watengenezaji wa magari hawataki kuzinunua.
Cars are not our primary interest. The automakers don’t want to buy them.
Alisema Dr Charles Stevens.
Alisema makampuni mengi ya magari yanataka kutengeneza pesa zaidi kwa kutumia engines za gas na kwamba itawachukua miongo kadhaa kukubali na kuanza kutmia teknolojia ya Thorium.

Endapo gari hili litafanikiwa kuingia sokoni na kununuliwa na watu wengi miaka ijayo, itakuwa hatari kwa biashara ya mafuta hasa kwa wale wanaotegemea magari pekee kufanya mauzo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527