JAMAA AENDA KUTAHIRI LAKINI MADAKTARI WAKATA UUME WOTE ,AFUNGUA KESI MAHAKAMANI


Mtu mmoja mjini Alabama nchini Marekani amefungua kesi ya madai baada ya kudai kuwa alikwenda kutahiriwa lakini madaktari wakaondoa uume wake wote.

Tovuti ya Metro imesema Johnny Lee Banks Jnr anadai kuwa alikwenda kufanya 'suna' katika hospitali ya Princeton Baptist Medical Center na uume wake kukatwa kimakosa na madaktari.

Kesi hiyo iliyofunguliwa na Bwana Banks pamoja na mkewe Zelda, inasema bwana huyo hakupewa maelezo yoyote ya kwanini 'mashine' yake iliondolewa na wala hakuonywa kuwa shughuli ya kutahiri ina hatari na uwezekano wa kukatwa kabisa uume.

 Mshtaki alipozinduka kutoka kwenye dawa ya usingizi baada ya upasuaji, alikuta uume umekatwa
yamesema maelezo ya mashtaka.
 Mdai hakutoa idhini yoyote ya kukata kabisa au nusu ya uume wake
imesema karatasi ya mashtaka.
Bwana huyo ameitaja hospitali, pamoja na madaktari wawili kuwa ndio washtakiwa katika kesi hiyo, akisema walikuwa wazembe na walishindwa kutafuta msaada walipopatwa na tatizo wakati wa upasuaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post