WAZUNGU WATANGAZA KIPINDI CHA TV KINACHOONESHA WANAWAKE WAKIJIFUNGUA PORINI

birth
Kampuni ya Lifetime ya nchini Marekani imetangaza kipindi kipya cha Televisheni kitakachoonyesha wazazi vijana wakijifungua porini bila msaada wa madaktari wakati wa hatua zote za kujifungua lakini pia hawatakuwa na malazi yoyote katika eneo hilo.
birth2
Kipindi hicho “Born in the Wild” kitatoa taswira kwa wanawake na wanaume ambao wanaamini kuwa kujifunga mtoto katika mazingira mazuri na kupatiwa huduma zote mbali na madaktari ni njia pekee.
birth3
Kipindi hicho kimetokana na video iliyopata umaarufu mkubwa katika mtandao wa YouTube na kutazamwa mara milioni 20 ikionyesha mwanamke akijifungua porini lakini tayari wakosoaji wa mambo wanasema kipindi hicho kinaweza kutoa taswira ya kuhatarisha maisha ya wamama na watoto wanaopitia mazingira hayo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527