Muda mfupi baada ya Luis Suarez kumng'ata Giorgio Chiellini begani, mitandao kijamii haikuchelewa kuzamisha meno yake kwa mshambuliaji huyo wa Uruguay. Suarez,aliyewahi kupigwa marufuku mara mbili kwa kuuma, alidaiwa kumng'ata mchezaji huyo wa Italia katika mechi ambayo Uruguay ilishinda 1-0. Picha mbalimbali za utani zimetengenezwa kutania tukio hilo na hizi ni miongoni mwao.