Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

TAZAMA PICHA-MASHINDANO YA UMIVUSTA KANDA YA MAGHARIBI YAFUNGULIWA RASMI SHINYANGA,YAANZA KWA KISHINDO JIONI YA LEO

Hapa ni katika uwanja wa chuo cha ufundi stadi cha VETA Shinyanga ambapo leo kumefanyika ufunguzi rasmi wa mashindano ya UMIVUSTA(Umoja wa Michezo kwa vyuo vya ufundi stadi Tanzania) lakini hapa ni kwa ajili ya UMIVUTA kanda ya magharibi inayojumuisha mikoa ya Tabora,Shinyanga,Kigoma na Simiyu ambapo mgeni rasmi alikuwa afisa tawala wilaya ya Shinyanga Charles Maugira aliyemwakilisha katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga.Mashindano hayo mwaka huu yatahusisha vyuo 8 kati ya 16 vilivyoalikwa ikiwa ni miongoni mwa vyuo zaidi ya 20 vya veta vilivyopo katika kanda ya magharibi.

Mratibu wa UMIVUSTA kanda ya magharibi Rodrick George akitambulisha wageni waliohudhuria ufunguzi wa mashindano hayo ambayo  mwaka huu yanashirikisha vyuo 8 ikiwa ni ongezeko la vyuo 3 tofauti na mwaka 2013.Idadi hii ya vyuo vinavyoshiriki inakutanisha wanavyuo wapatao 160 na walimu 16 ikilinganishwa na wanavyuo 100 na walimu 10 walioshiriki mwaka 2013.

Walimu zaidi ya kumi kutoka vyuo vinavyoshiriki mashindano hayo wakitambulishwa leo katika viwanja vya Veta Shinyanga mjini Shinyanga.Vyuo vinavyoshiriki mwaka huu ni  Veta Ulyankulu,Nzega Fdc,Veta Urambo,Veta Tabora na Tabora Network kutoka mkoa wa Tabora,kutoka Shinyanga ni Veta Shinyanga na Buhangija fdc,kutoka Kigoma ni Veta Kigoma na mkoa wa Simiyu haujaleta chuo.
Aliyesimama ni mkurugenzi wa VETA kanda ya Magharibi Hildegardis Bitegera Bana akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya UMIVUSTA kanda ya magharibi ambapo alisema michezo hiyo ilianzishwa mwaka 1996 hapa nchini lakini kanda ya magharibi mwaka 2007 ikiwa na lengo la kuwakutanisha vijana wanaosoma katika vyuo vya ufundi mbalimbali nchini ili waweze kuonesha viapaji vyao katika michezo ikiaminika kuwa kwa kupitia michezo hiyo vijana hao wangeweza kubadilishana uzoefu na kujenga urafiki na ushirikiano miongoni mwao,kujenga afya bora ya akili na mwili ili kumudu vyema masomo yao kiufundi.
Aliyesimama ni mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa mashindano ya UMIVUSTA kanda ya magharibi ambaye alikuwa afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga ndugu Charles Maugira ambapo aliwaka vijana hao kutumia fursa waliyopewa ikizingatiwa kuwa sera ya taifa la Tanzania kwa sasa ni kukuza michezo kwenye taasisi za elimu ili kupata vijana wenye nidhamu na nguvu.Aliongeza kuwa michezo hujenga furaha na ushirikiano na kichocheo muhimu katika kujifunza na kwamba sasa hivi michezo ni ajira yenye ujira bora zaidi.
Wadau wa michezo wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi 

Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga ndugu Charles Maugira akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya UMIVUSTA ambapo michezo ya aina nne imeanza kufanyika leo katika viwanja vya Veta mjini Shinyanga.Michezo hiyo itafanyika kwa siku kumi kuanzia leo na michezo itakayofanyika ni mpira wa miguu,pete,mpira wa wavu na riadha kwa mbio fupi.
Wadau wa michezo wakiwa katika viwanja vya Veta Shinyanga leo jioni
Mgeni rasmi Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga ndugu Charles Maugira (mwenye kofia mbele) akikagua timu ya mpira wa miguu ya  VETA Shinyanga(wenye jezi za njano),nyuma yake ni mkurugenzi wa VETA kanda ya Magharibi Hildegardis Bitegera Bana  akifuatiwa na mkuu wa Chuo cha VETA Shinyanga bwana Afridon Mkhomoi ambaye ndiyo mwenyeji wa mashindano ya UMIVUSTA kanda ya magharibi mwaka 2014
Mwenye suti ni mkuu wa Chuo cha VETA Shinyanga ndugu Afridon Mkhomoi akishikana mikono na wachezaji wa timu ya Veta Tabora pamoja na waamuzi wa mchezo uliokuwa unafuata,aliyeshikilia kitabu ni Mratibu wa UMIVUSTA kanda ya magharibi Rodrick George 
Timu kati ya veta Shinyanga(kulia) na timu ya Veta Tabora (kushoto) zikiwa uwanjani kabla ya mechi kuanza ikiwa ni mechi ya pili kwa siku ya leo ya kwanza ilikuwa kati ya timu ya mpira ya Veta Nzega vs Tabora Network ambapo mshindi alikuwa Veta Nzega walioibuka na ushindi wa bao 2-1
 Timu ya Veta Tabora ikiwa uwanjani kabla ya mchuano wake na timu ya veta Shinyanga
 Timu ya mpira wa miguu ya veta Shinyanga ikiwa uwanjani kabla ya mechi


 Mechi kati ya Veta Shinyanga na Veta Tabora ikiwa inaendelea ambapo hadi mwisho wa mchezo Veta 0 huku Veta Tabora-1
 Tunaangalia mechi...........

 Mchezo unaendeleaa
 Tunashangiliaaaa



 Tunashuhudia mechi....

Michezo ya UMIVUSTA ilifanyika moja kwa moja katika ngazi ya taifa hadi mwaka 1997 ambapo michezo iliamuliwa ichezwe kwenye ngazi ya kanda na baadaye ndiyo iendelee kwenye ngazi ya taifa,na kanda ya magharibi imenza kufanyika mwaka 2007 na mwaka huu 2014 ni mara ya 3 ya kufanyika.

Katika kufanikisha mashindano hay Vyuo shiriki vimechangia gharama za usafiri na chakula kwa wanavyuo wao ambapo ofisi ya veta kanda ya magharibi imegharamia ununuzi wa sare za michezo kwa ajili ya ufunguzi,gharama za waamuzi wa michezo yote,pia imenunua mipira yote,zawadi kwa washindi,masurufu ya mratibu,gharama za maji,umeme na kuni n.k

Gharama za huduma ya kwanza zimendaliwa na ofisi ya mkurugenzi wa kanda ambapo jumla kuu ya gharama zilizotumika na zitakazoendelea kutumika hadi mwisho wa mashindano hayo ya umivusta ni shilingi 8,292,500/=


PICHA ZOTE NA KADAMA MALUNDE-MALUNDE1 BLOG- SHINYANGA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com